Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Thursday, December 29, 2022

SEHEMU YA TATU MAKALA YA MWELEKEO WA MANISPAA YA MORO KUWA JIJI CHEKI PICHA ZA VULUGU BARABANI.

                                       Kibao cha zuio






Vulugu tupu licha ya soko kuu la Manispaa Maarufu soko la Kingalu kuwa jirani na eneo hili kama umba wa nusu ya kiwanja cha Mpira wafanya biashra hawa wa bidhaa za sokoni wakifanya biashara eneo hili la barabara mbele ya madua ya watu. wenye magari licha ya kibao cha kuwazuiA Kuegesha magari wameegesha na kununu bidhaa eneo hili kama Jamaa akuludi na fenesi lake baada ya kushindwana bei na mmoja wawateja aliyeegesga gari eneo hili

Hatari sana jamaa akichoma mahindi katikati ya barabara ya Makongoro makutano la barabara 4 zenye mzongamano mkubwa wa magari. kufuatia hali hiyo baadhi ya wananchi waliomba eneo hilo kufungwa taa za kuongozea magari licha ya hari hiyo wafanyabiasha hawa wameketi kabisa kwenye kona

 


Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

Takribani siku tatu mfurulizo Mwandishi wa Mtandao huu amejikita kwenye habari ya uchunguzi wa Manispaa ya Morogoro kuwa jiji.

 

Jana Mwandishi huyo aliahadi kutupia picha za wafanyabiashara ndogo ndongo’Wamachinga’ wakiwemo kina mama wauza mboga mboga pamoja na madereva wa Bajaj kwa pamoja wakijazana katikati ya Mji wakivunja  sheria na kuufanya mji huo  kukosa mpangilio hivyo kupoteza baadhi ya Vigezo vya kuwa jiji.

 

Wafanyabiashara hao walipanga biashara zao barabani hali iliyopelekea usumbufu kwa vyombo vya Moto na watu wanaotembea kwa miguu wakiwemo Walemavu,kwa upande wa madereva wa Bajaji nao wanavunja sheria kwa kushusha na kupakia abiria ndani ya kituo cha Mafuta, kama hiyo haitoshi Bajaj hizo pia hushusha na kupakia abiria ndani ya kivuko cha watembea kwa Miguu’Bums ya stend ya zamani ya Daladala.

 

 Vile vile baadhi ya Bajaj hizo hushusha na kupakia abiri ndani ya Mzunguko wa barabara za Madaraka inayoelekea SUA. Barabara ya Boma, inayoelekea ofisi ya Mkuu wa Mkoa, barabara ya Korogwe inayoelekea Msamvu na barabara ya zamani ya Dar es salaam inayoelekea Bigwa.

 

Cha kushangaza licha ya Mamlaka husika kuweka kibao cha zuio la Bajaj kupitia eneo hilo kuwepo kwenye  mzunguko huo wa barabara bado madereva hao wa Bajaj wameonegaka kukaidi  amari hiyo.

 

 Leo jioni  Mwandishi huyo wa habari za kichunguzi aliwanasa madereva hao wakishuka kwenye Bajaj zao na kugombea abiria ndani ya Mzunguko huo wa barabara jirani  kabisa  na kibao hicho cha zuio  bila wasiwasi wowote.

 

 Bajaj nyingine zikionekana zikishusha na kupakia abiria ndani ya kituo cha Mafuta jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa abiri na vyombo vyao.

 

 Sheria za usafirishaji zinazuia Vyombo vya Moto kuingia kituo cha mafuta kujaza mafuta huku kikiwa na abiri.

 

Masikini ya Mungu wakati Shushu huyo wa habari  za kichunguzi anayetumia kamera za kisasa zenye uwezo wa kupiga Picha usambali Mrefu ambazo pia hazito Mwanga alimshuhudia Mlinzi wa Kituo hicho cha Mafuta akipuuzwa na madereva hao wa Bajaj.

 

 

Shushu huyo akiwa umbali wa zaidi ya Mita 200 akipiga Picha Bajaj hizo zikiwa ndani ya kituo hicho cha Mafuta alimshuhudia Mlinzi huyo akihangaika kuzifukuza Bajaj hizo bila Mafanikio.

 

 Licha ya Mlinzi huyo kuwafukuza Madera hao walimpuuza na kuendelea kushusha na kubakia abiri kama Picha zinavyoonyesha Mlinzi huyo akiwafukuza bila mafanikio.

 

Baada ya kupiga Picha hizo za kishushu akiwa umbari mrefu,Mwandishi huyo aliludisha Kamera kwenye begi na kutinga kwenye kituo hicho cha Mafuta na kuzungumza na Mlinzi huyo ambapo alipotakiwa kueleza hali hiyo alisema.

” Bora Mwandishi wa habari nisaidie hawa madereva wa Bajaj wanataka kunifukuzisha kazi bosi wa Kituo hiki kapiga marufuku Bajaj kushusha na kupakia abiria ndani ya kituo chake akitupa agizo sisi walinzi  kuhakikisha Bajaj hazifanya hivyo”alisema Mlinzi huyo na kuongeza kudadavua.

 

Kama unavyoona wanafukuza hawasikii wanaendelea kushusha na kupakia abiria eneo hili”alisema Mlinzi huyo aliyeomba hifadhi ya jina lake kwa sababu yeye  si msemaji wa kituo hicho.

 

Mwandishi huyo alipotaka kuzungumza na bosi wa kituo hicho Mlinzi huyo alidai kwa muda huo wa saa 12 jioni ameshatoka ofisini hivyo.juhudi hizo za kumtafuta zinaendelea.

 

Mara baada ya kuzungumza na bosi huyo Mwanahabari huyo  pia atatinga Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro’RPC’kuzungumza naye kuhusiana na vulugu hizo za Bajaj  ambazo nyingi hazina namba ya Usajiri nyuma kama zinavyonekana Pichani.

 

Mwandishu huyo pia atatinga ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa kwa lengo la kupata maelezo ya Wamachinga hao kuzagaa barabarani huku baadhi wakiwasha Moto na kuchoma mahindi katikati ya barabara.

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...