Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Saturday, December 31, 2022

SEHEMU YA 3 MAKALA MAALUMU MANISPAA YA MORO KUWA JIJI. MKURUGENZI NA RPC WAFUNGUKA.

  

Mwandishi wa Mtandao huu akizungumza na RPC Muslimu.



 Kulia Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro Ally Machelle.


 

Na Dunstan Shekidele, Morogoro.

 

KWA takribani wiki moja sasa Mwandishi wa Mtandao huu amejikita kufanya uchunguzi Maalumu wa kuelekea Manispaa ya Morogoro kuwa Jiji.

 

 Mengi yameelezewa kwenye Stori za nyuma ambazo bado ziko kwenye Mtandao huu Pendwa nchini na kwamba stori ya Mwisho Mwandishi  aliahadi kuwatafuta Mkurugenzi wa Manispaa na Kamanda wa Polisi;RPC’ kwa lengo la kuwahoji vigogo hao ili watupatie majawabu ya baadhi ya kero zinazoendelea kwenye Manispaa hiyo.

 

Jana Mwandishi huyo wa habari xa kiuchunguzi aliwasaka Vigogo hao na kufanikiwa kuwapata wa kwanza kupatikana alikuwa RPC Fortunatus Musilim  alipoelezwa kero ya Bajaj kupakia na kushusha abiri maeneo ya sio lasimi ikiweno ndani ya kituo cha Mafuta.

 

Big boss huyo wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro alisema, “ Ni kweli  hali hiyo ilitokea siku za nyuma tukazungumza na madereva hao wa Bajaj kuhusiana na kushusha na kipakia abiria walitueleza kwamba pale kituo cha mafuta wanaingia kujaza mafuta tu na sio kushusha na kupakia abiri.

 

 Kamanda huyo alipoulizwa kama sheria inaruhusu chombo cha Moto kujaza mafuta abiria wakiwa ndani RPC Musilim alijibu” Hiyo hairuhusiwi nikuombe shekidele uniachie swala hili nitalifanyia kazi”alijibu Kamanda huyo.

 

Baada ya kutoka kwa RPC Mtandao huu ulitinga kwa Mkurugenzi wa Manispaa Ally Machela na mahojianoi yalikuwa hivi.

 

Mwandishi- Pole na majukumu ya kujenga taifa letu bosi.

Mkurugenzi. Asante sana Mwandishi pole na wewe kwa majukumu ya kutuhabarisha.

 

Mwandishi. Asante sasa bosi sasa Mwaka umekwisha ule mpango wetu wa Manispaa ya Morogoro kuwa Jiji umefikia eneo gain?

 

Mkurugenzi. Unaelekea Vizuri na kwa sasa kama ulivyoona tumebandika Vipepelushi vya kuhamasisha ushaji ili Mji wetu uwe safi.

Mwandishi. Unahakika kazi hiyo ya usafi inafanyika vizuri?.

 

Mkurugenzi.lnafanyika vizuri.

 

Mwandishi. Sio kweli Mkuu haifanyiki vizuri ni kweli vijana wako wako kazini kufanya usafi ikiwemo kusafisha mitaro ya barabarani kazi hiyo haifanywi vizuri naweza kusema ndio kwanza hali hiyo inachafua Mji.

 

Mkurugenzi. Kwa nini unasema hivyo.

 

Mwandishi. Nasema hivyo kwa sababu Vijana wako wanatoa tope zito kwenye mifereji hiyo na kulitupia katikati ya barabara tena eneo la maduka ya watu wakiwemo kina Mama Ntilie jambo ambalo ni hatari kwa afya za wateja wao.

 

Mkurugenzi. Eneo lile la barabara za Nane Nane na Kola ziko chini ya wenzetu wa TARURA na Picha zile niliziona tumewasiliana na wenzetu wa TARURA nadhani siku mbili hizi watakwenda kuzoa tope lile pale barabarani. 

 

Mwandishi. Sasa kama hali ndio hii nyinyi wahusika mnatoa tope kwenye mifereji na kulitelekea barabarani ndoto zetu za Manispaa wetu kuwa jiji zitatimia kwa uzoaji taka huu wa kizamani?. Mkurugenzi. Nimekwambia eneo lile ni la TARURA. Mwandishi. Any way tutoke huko je kuelekea Manispaa kuwa Jiji inapaswa wafanyabiashara ndogo ndogo’Machinga’ watengewe maeneo maalum wasizagae hovyo Mjini.

 

Nyakati za  Jioni wamachinga wengi wanapanga bidhaa  barabarani hasa barabara za  Madaraka eneo la Lunna na ile ya Boma jirani na Msikiti Mkuu.

 

 Mkurugenzi. Ni kweli inashangaza asilimia 75 ya hao wamachinga tumewapa Vibanda soko Kuu la Kingalu na Soko la Faya lakini wametoka kule na kurejea barabarani kwa sababu ni wananchi wetu tunaendelea kuwapa elimu ili waondoke kiastaarabu.

 

 Wewe Mwandishi unakumbuka ile barabara ya Boma pale jirani na Msikiti ilitokea ajari gari imeacha njia imewavamia kina mama waliokuwa wakiuza bidhaa zao barabarani tulitumia Mgambo kuwaondoa baada ya wiki wamerejea tena.

 

 Mwandishi. Swala la kupanga biashara barabarani ni kosa kisheria sasa tukienda kwa mfumo huyo kuwabembeleza wamachinga kutoka barabarani Manispaa yetu itachelewa sana kuwa Jiji. Mimi kama Mwandishi naona kama kweli tunadhamira ya dhati Manispaa yetu kuwa Jiji tuache Siasa tusimamie sheria Mtu katupa takataka faini elfu 50. Mmachinga katoka kwenye eneo alilopangia kaja barabara anakamatwa faini elfu 50 ndio Majiji ya wenzetu wanavyofanya.

 

Mkurugenzi. Sawa. Mwandishi. Asante kwa ushirikiano wako.

 

Makalla yetu ya Kuelekea Manispaa ya Morogoro kuwa jiji inaishia hapa. Shekidele hana hatia ametimiza Majukumu yake Kama Mwana Morogoro na Mwandishi wa habari kuwakumbusha Viongozi na wananchi wenzake.

                             

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...