Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Saturday, December 24, 2022

KUMBUKIZI YA KUZALIWA,MWANDISHI AOMBA RADHI.

Mesia Yesu Kristo akizaliwa katika Zizi la Ng'ombe Desemba 25
Dunstan Peter Shekidele alizaliwa hospital ya  ya Rufaa ya Bombo Jijini Tanga Desemba 25

 


                 Na Mwana Birthday Dunstan Shekidele.

Leo Desemba 25 Wakristo duniani kote wanasheherekea siku kuu ya kuzaliwa Mesiha Yesu Kristo ambaye Mungu alimtoa kama sadaka kwa wanadamu, aliluhusu Mtume huyo aliyekuja kuukomboa Ulimwengu azaliwe katika zizi la kufungia Ng’ombe kama picha ya mfano inavyoonyesha Mtoto Yesu akizaliwa katika Zizi hilo la Ng’ombe.

Leo Pia Decemba 25 ni kukumbizi ya Kuzaliwa kwa Mwandishi wa Mtandao huu ambaye yeye hakuzaliwa Katika Zizi la Ng’ombe bali amezaliwa katika Hospital ya Rufaa ya Bombo iliyopo kando kando ya Bahati  Jijini Tanga.

 

              SHUKRAN.

Kipekee na Msukulu Mungu kwa kuendelea kunipa zawadi ya Uhai na leo hii kwa Neema zake ameniongezea Mwaka Mwingine.

Pili nawashukuru wazazi wangu Marehemu Baba yangu Mzee Peter Zakari Shekidele Mungu amepe punziko   la Aman.

Tatu. Mama yangu Kipenzi Tumaini Samwel Juma ‘Mrs Shekidele’ anayeendelea na Matibabu jijini Dar es salaam na Muombea kwa Mungu amponye upesi.

Nne nawashukuru Viongozi wote wa dini zote kwa kuendelea kutupa mahubiri na Mawaidha yenye lengo la kutuweka karibu na Mwenyezi Mungu.

 

 Tano. Nawashukuru Viongozi wote wa Serikali ya Jamhuri ya Mungano wa Tanzania kwa kuenzi na kudumia Amani inayopelekea mimi na wananchi wengine kuishi kwa amani.  

Sita. Nawashukuru ndugu zangu Marafiki zangu na wadau wote wa Mitandao yangu ya Kijamii hasa Facebook.                        MSAMAHA.

Kupitia siku yangu hii ya kuzaliwa naomba Msahama wa dhati toka ndani ya sakafu ya Moyo wangu kwa mtu yoyote niliyemkosea kwa kujua ama kwa kutoa kujua naomba anisamehe kwani mimi ni kiumbe dhaifu si Mkamilifu.  

 

Pia kupita siku hii nimewasamehe kwa dhati  wote walionikosema kwa namna yoyote ile.

Happy Birthday Yesu Kristo, Happy Birthday Dunstan Shekidele, Happy Birthday watu wote waliozaliwa siku  ya leo Desemba 25.

               UJUMBE KWA WOTE.

Kumcha  Bwana’Mola’ ndio chanzo cha Maarifa. Hapa duniani tunapitia kuna maisha mengine tena mazuri zaidi ya maisha haya ya duniani yaliyojaa damu na shida nyingi.

 

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...