Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Monday, December 26, 2022

HAPA SIO ULAYA NI MJI KASORO BAHARI.



 


 

 Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

Kama kichwa cha habari kinavyoeleza hapo juu ni kweli Mijengo hiyo haiko Ulaya bali iko Maeneo la Msamvu Mkoani Morogoro.

 

 Maghorofa hayo ni hotel za kisasa ambapo Mwandishi wa Mtandao huu si kama anatoka kula bata kwenye hotel hizo hapana  anatoka  kufanya kazi yake ya Uandishia wa habari.

 

Kwa sasa Mji wa Morogoro unazidi kukua kwa kwa kasi ambapo aliyekuwa rais wa awamu ya 5 hayati John Pombe Magufuli’JPM’ wakati akizindua Soko kuu la Kisasa la Morogoro Maarufu Soko la Chief Kingalu.

 

Alishangazwa Manispaa ya Morogoro mpaka sasa kutokizi Vigezo vya kupewa hadhi ya Jiji ili hali mikoa inayolingana na Manispaa hiyo kama Mkoa wa Tanga na Dodoma kukidhi Vigezo vya Jiji huku Morogoro ikishindwa kufanya hivyo.  Kwa Miaka Mingi kufuatia ukubwa wa Mji wao wenyeji wa Mkoa wa Morogoro’Waluguru’wanakausemi kao kanakosema ”Mweee Morogoro Mji Kasoro Bahati Tu” Uchunguzi wa awari uliofanywa na Mwandishi wa habari hizi umebaini baadhi ya vigezo vinavyopelekea Mji huo kukosa Vigezo vya Manispaa ni Pamoja na Chafu wa Mji  wamachinga kuzagaa hovyo katikati ya Mji.

 

 Kuhusu Uchafu Mfano Juzi  Mwandishi wa Mtandao huu alikatiza  barabara mpya za kisasa za Viwango vya lami chaajabu baadhi ya wafanyakazi wa Manispaa kwa sasa wanaendelea kutoa tope zito kwenye mifereji na kutupa katikati ya barabara ya lami.

 

 Tope hilo lipo zaidi ya siku 4  bila kuzolewa na hivyo barabara hio 2 ile inayotoka Nane nane kuelekea Makaburi ya Kolla na ile inayotoka Nane nane eneo la Maegesho la Malori inayoelekea Kichangani kugeuka kuwa ya vumbi ili hali chini kuna lami.

 

 Muda huu napita tena kwenye eneo hilo kama nikikuta tope hilo bado halijazolewa nitapiga Picha na kurusha hewani kwa lengo la kuwakumbusha Vigogo wa Manispaa.

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...