Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Friday, December 23, 2022

KUMBUKIZI YA KIFO CHA BIBI WA MIAKA 103

Picha no 2 Mwinjilisti wa kanisani la KKKT Usharika wa Kitunda Dar akiongoza lbada fupi ya kumuombea Marehemu ndani ya Hospital ya Amana kabla Mwili wa Mpendwa wetu kusafirishwa kuelekea Lushoto kumpunzisha kwenye nyumba yake ya Milele.


Jeneza lililo beba mwili wa bibi Kete likiingizwa kwenye gari tayari kwa safari ya kuelekea kijijini kwake  Tarafa ya Mlalo  Wilaya ya Lushoto Mkoani Tanga. Picha juu ni baadhi ya familia ya bibi Keke inayosihi jijini Dar es salaam wakishiriki lbada fupi iliyofanyika hospitalini hapo
Msafara huo ukikatiza maeneo mbali mbali ya jiji la Dar ukielekea Lushoto ukipitia njia ya Bagamoyo Road ambapo Mpiga Picha wa Mtandao huu aliyeketi siti ya mbele ya moja ya Coaster alifanya kazi ya kupiga Picha matukio yote ya njiani
....Msafara huo ukiwasili daraja la Wami barabara kuu ya Calinze Segera


Msafara huo ukiwasili Stend ya Mkongoloni Jimbo la Mlalo Lushoro
William Peter Shekidele ambaye ni Mjukuu wa kwanza wa bibi kete akizungumza na anko wake David Juma kulia ni Dkt lkunda Riwa kitukuu cha marehemu ambaye pia ni mtoto wa kwanza wa Elice Peter Shekidele

Changamoto mwenzi huo wa Desemba ni mwezi wa msimu wa Mvua ambapo basi lililobeba mwili wa marehemu lilikwama kwenye moja ya barabara za kijijini hapo na kurazimika waombolezaji kutoa msaada wa kulisukuma na kufanikiwa kuvusha eneo hilo korofi
Msafara huo ukiwasilia nyumbani kwa mume wa marehemu Mzee Samwel Juma ambaye pia alitangulia mbele za haki

Kutoka Kulia Dustan Peter Shekidele, Elisante Peter Shekidele Wiliam Peter Shekidele wakiwa na Anko wao David Juma mwenye kofiakati] wa mwisho kushoto ni Mpiga kinanda maarufu wa kanisa la KKKT Usharika wa Mlalo ambaye pia anaudugu na familia hiyo ya Marehemu.
                     Kanisa la KKKT Usharika wa Mlalo
David Juma ambaye ni Mtoto pekee wa kiume wa Marehemu akimlilia Mama yake hulia anayembendeleza ni Mke wa David Juma
Mwili wa bibi Kete ukitolewa kanisani baada ya kumilika kwa lbada


Msafara ukitoka kanisani ukielekea nyumbani kwake msafara huo ukiongozwa na matarumbeta ya kanisa la KKKT Usharika wa Mlala ambapo enzi za Uhai wake bibi Kete Abdallah alikuwa Mwana kwaya ya kwaya Kuu ya Usharika huo
;;;Mwili ukiwasi kwenye nyumba yake ya Milele

Anko David Juma akiwa kwenye kaburi la Mpendwa mama yake mara baada ya kumzika kwenye shamba lake Mlalo Lushoto Picha zote na Dunstan Shekidele aliyekuwa Lushoto

...Msafara huo Ukiwa Lushoto Mjini ukirejea Dar es salaam baada ya mazishi
Kutoka Kushoto Dustan Peter Shekidele, William Peter Shekidele na Elisante Peter Shekidele Kwa pamoja wakiwa kwenye kaburi la Mpendwa baba yao hayati Peter Zakaria Shekidele, kaburo hilo liko nje ya kanisa la KKKT Usharika wa Mlalo Lushoto.
...Hayati Bibi Kete Abdallah103' enzi za uhai wake lfahamike licha ya kuw ana umri huo Mkubwa bibi Kete alikuw aakisumbuliwa na Miguu tu lakini hajawahi kusumbuliw ana ugonjwa wa Pesha kisukari wala ugonjwa wowote na hadi anafariki alikuw aakisoma biblia ba sms kwenye simu bila kutumia miwani
Bibi kete akimpa wosia Mjukuu wake ambaye ni Mwandishi wa Mtandao huu kwa Lugha ya Kisambaa
Vicky David Juma Mjukuu akimsaidia bibi yake kukata keki kwenye moja ya Birthday zake.

KUMBUKIZI.

Leo Desemba 22 Mpendwa wangu. Mke wangu, Kipenzi cha Moyo wangu, barafu wa Moyo wangu, My Number One, Mshauri wangu, Msili wangu.

 

Kette Abdallah umeniacha mpweke baada ya kutwaliwa na Bwana ukiwa usingizini nyumbani kwako Gongolamboto,Mombasa, Mtaa wa Moshi Baa jijini Dar es salaam.

 

Marehemu Kete ambaye ni bibi yangu aliyenizalia Mama yangu Mzazi alifariki dunia Desemba 22 2019 akiwa na umri wa Miaka 103.

Marehemu ameacha watoto watatu Tumaini Samwel Juma, ‘Mrs Shekidele’, David Samwel Juma na Neema Samwel Juma’Mrs Mulokozi’ Wajukuu, Vitukuu na Vilembwe zaidi ya 100.

 

Pichani Bibi Kette akinipa wosia kwa Lugha ya Kisambaa kwenye moja ya sherehe zake za kuzaliwa’Happy Birthday iliyofanyika nyumbani kwake Moshi Baa.

 

Leo Desemba 22 2022 ametimiza miaka 3 toka alivyofariki dunia na kuzikwa kijijini kwake Mlalo Wilaya ya Lushoto Mkoani Tanga Desemba 26.

 

Watu wengi walihoji sababu za kuchelewa kuzikwa na Mpendwa wetu, nami na wajibu kwamba sababu ya msingi ya kuchelewa kumzika Mpendwa wetu ni kwa sababu ya kumsubiri mwanae pekee wa kiume David Juma anayeishi Marekani.

 

Bwana ametoa na Bwana ametwa jina lake lihimidiwe.

 

Umetangulia bibi yangu tutaonana baadae.

  

 

 
 

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...