Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Tuesday, October 25, 2022

YARIYOJIRI KUMBI ZA STAREHE MWISHONI MWA WIKI. WANENGUAJI WATIMULIWA KWENYE BAND KWA UTORO KAZINI.

Sabrina akitamburishwa kwenye band ya Maisha Mapya akitokea band ya Waluguru.



 Sabrina akiwajibika  wiki iliyopita baada ya kureja band yake ya Waluguru


Mourine V.A.R akiwasha Moto kwenye Jukwaa la Maisha Mapya. kabl ya kutimuliwa kwenye band hiyo kwa sababu za Utoro kazini.

Wanenguaji wa band ya Waluguru wakiuwasha Moto  nyuma yao ni Sabrina akishriki kwenye shoo hiyo


Rap Mahiri wa band ya Waluguru Og Mudizo akiwakoreza wanenguaji wa band Wanengauji wa band ya Waluguru wakiwajibika Jukwaani

Safu ya Waimbaji wa band ya Waluguru wakiwajibika Jukwaani



Mnenguaji nyota wa band ya Waluguru Og Sinyorita akifanya yake wiki end iliyopita





 

 

Na Mlala Nnje Dunstan Shekidele,Morogoro.

 

HII Kali Wanenguaji wawiki nyota wa kike wa band ya Maisha Mapya, Sabrina Danger na Mourine V.A.R wamefukuzwa kwenye band hiyo kwa sababu za utoro kazini.

 

Mwishoni mwa wiki iliyopita Mlala Nnje akiwa kwenye Pilika pilika  za kusaka matukio usiku mnene kwenye kumbi mbali mbali za Starehe alikatiza kwenye shoo ya band ya Waluguru Origanal katikati ya Mji wa Morogoro na kumshuhudia Mnenguaji Sabrina Danger akiuwasha Moto na Waluguru hao.

 

lfahamike hivi karibuni Sabrina aliikacha band hiyo ya Waluguru na kutimkia band Pendwa ya Maisha Mapya, wadau wa Mtandao  Pendwa wa Shekidele watakumbuka siku alipotambulishwa takribani Miezi 2 iliyopita Mlala Nnje aliripoti habari hiyo.

 

Sabrina alivyoshuka Jukwaani Mlala nje alimfuta na kumuliza kulikoni ameikacha band ya Maisha Mapya na kurejea band yake ya zamani ya Maisha Mapya?alicheka kisha akajibu kwa mkato “Nimerejea nyumbani wale Jamaa zako hawanaishu”.

 

Usiku huo huo Mlala Nnje kapiga Gia Pikipiki yake ya Mwendokasi hadi kwenye shoo ya band ya Maisha Mapya maeneo ya Mazindu na kuzungumza na Kiongozi wa band hiyo Joshua Malekela ambapo alipoulizwa juu ya mnenguaji huyo alijibu kwa Jazba.

 

”Tumewafukuza wanenguaji  Sabrina na Mourine kwa sababu ni watoro kazini eti Sabrina akiwa na matatizo Mourine haji kazini wiki inayofuta Mourine akiomba ruhusu, Sabrina naye hajikazini sasa hatuwezi kuwavumilia wanamuziki wa sampuli hiyo wanaoleta utani kwenye kazi”alisema Malekea.

 Mourine V.A.R naye alijiunga na band hiyo hivi karibuni akitokea band ya Afrikan Stars’Twanga Pepeta’ ya Jijini Dar.

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...