Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Friday, October 28, 2022

TAARIFA

Never'Kamwe' Penzi la Mama haliishi nimevutiwa na maandishi ya Khanga hii hivyo moja ya zawadi nilizombebea Bi mkubwa ni pamoja na Khanga hii yenye ujumbe mzuri
Mwandishi wa Mtandao huu muda huu akiwa kituo cha Mafuta Chalinze Mkoa wa Pwani

 

TAARIFA.

Wadau wa Mtandao Pendwa wa Shekidele, takribani siku tatu sijaposti habari yoyote kwenye ukurasa huu,jambo ambalo sio kawaida.

 

Hii nimetokana na Mimi kwenda Dar es salaam juzi kumjulia hali Bi Mkubwa wangu aliyekuwa akisumbuliwa na maradhi mbali mbali ikiwemo Malaria.

 

Mungu ni Mwema kwa sasa Mpendwa Mama yangu kipenzi aliyenileta hapa duniani amepata nafuu,muda huu niko hapa Chalinze naongeza Mafuta niendelee na safari ya kurejea Morogoro.

 

Hivyo maombi yenu yanahitajika ili niweze kufika salama niendelee na majukumu yangu ya kuwahabarisha wadau wa Mtandao Pendwa wa Shekidele.

 

Kuna watu walivyoniona na gari hiki jipya Dar na Moro walinipongeza wakihisi ni Mali yangu ukweli ni mwamba gari hili si Mali yangu  ni mali ya rafiki yangu aliyenisaidia kwani kwenye safari hii niko na ndugu yangu Mlemavu wa Miguu ambaye kupanda kwenye ngazi ndefu za basi kwake ni changamoto kubwa.

Naamini bila ufafanuzi huu  hapa humu kwenye Mtandao watu wengi wangeamini kwamba chombo hii ni mali yangu jambo ambalo sio kweli.

Nafurahi Mali sina lakini nimejaliwa kuwa na rasilimali watu, naamini hii ni mali kubwa kuliko mali nyingine.si dhani kama inafaida kuwa na mali za duniani huku hunamahusiano mazuri na watu wakiwemo majirani zako.

 

 

 

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...