Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Thursday, September 15, 2022

YARIYOJIRI KUMBI ZA STAREHE MWISHONI MWA WIKI. BAND ZA MAISHA MAPYA NA WALUGURU OG, KAMA SIMBA NA YANGA.

Wanenguaji wa Waluguru Og wakiwajibika juzi jumapili


Rapa wa band hiyo Jonhcena Sukari akiwajaza mzuka wanenguaji
Mpiga Tumba nyota wa band hiyo Baloteli alipoona kamera za Mlala Nje kaweka pozi kama yuko Location








Prezedaa wa band ya Waluguru Killer Boy mwenye nguo nyeusi akiongoza safu ya waimbaji wa band hiyo juzi jumapili


Hawa sio TMK Wazee wa Mapanga shaa huyu ni mnenguaji fundi wa band ya Waluguru Original akifanya yake ile ile


Mnenguaji Kipenzi cha wana Morogoro Sinyorita akiwajibika jukwaani wiki end iliyopita





 

Na Mlala Nje Dunstan Shekidele,Morogoro. 

Band kubwa mkoani Morogoro Waluguru Original inayomilikiwa na Jeshi la Mtu mmoja Deogratius Aruphonce Maarufu ‘Killer Boy’na Band ya Maisha Mapya inayomilikiwa na jeshi la watu wawili  Joshua Malekele’na Abubakar Pugi wameingia katika vita ya kuchukuliana wanamuziki kama timu za Simba na Yanga.

 

 lkumbukwe miaka ya hivi karibuni Mchezaji Bernard Morrison alitoka Yanga na Kujiunga na Simba kabla ya Msimu huu kutoka Simba na kureja nyumbani Yanga.

 

Wiki mbili zilizopita Mlala nje alishuhudia band ya Maisha Mapya ikimtambulisha Mwimbaji wa kike kutoka band ya Waluguru Og, juzi jumapili Mlala nje alitinga kwenye shoo ya Waluguru Og na kushuhudia Mpiga bess Maarufu wa band ya Maisha Mapya Samwel Maarufu ‘Sam Bass’akiwajibika kwenye jukwaa la band hiyo.

 

 Mlala nje alimvaa mpiga bass huyo ambapo alipohojiwa alisema” Shekidele kwa sasa nimejiunga na Waluguru nimewakimbia Maisha Mapya nimekuja huku kutafuta changamoto Mpya za kimaisha”. Alisema Samu.

 

Usiku huo huo Mlala nje alimvutia waya Joshua Maarufu Joshkera ambapo alipoulizwa alithibitisha Sam kutimka kwenye band yake.

 

 “ Ni kweli Shekidele  Samwel sio Mwanamuziki wetu tena nafasi yake  tumempata mkali wa bass nchini Papaa Sembuche” alisema kiongozi huyo Maisha Mapya Wana ‘Full Vipaji.

 

 Katika shoo hiyo ya Waluguru kama kawaida wanenguaji nyota wa band hiyo wakiongozwa na Mrembo Sinyorita waliuwasha moto mkali na kukong’a nyoyo za mashabiki kibao waliofulika kwenye ukumbi  huo wa Florida uliopo jirani na Stend ya Mabasi ya Mikoani ya Msamvu.

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...