Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Saturday, September 24, 2022

YANGA, SIMBA WAONDOA TOFAUTI ZAO WAUNGANA KUSAIDIA FAMILIA MOROGORO.

Wanachana wa Yanga na Simba wakitoka tawi kuu la Simba Mkoani Morogoro wakielekea kukabidhi Misaada wa kaya 9
Mhasibu Msaidizi wa tawi la Simba Maarufu tawi la Shujaa Ngome Kuu Mogella 'DHL'akiteta jambo na Mwenyekiti wa tawi kuu la Yanga lssa Chabala huku wakielekea eneo la tukio








...Wenyetivi wa matawi ya Simba na Yanga Said Mkwinda wa kwanza kushoto mwenye jezi ya Simba na lssa Chabala mwenyekiti wa tawi kuu la Yanga wakimkabidhi madaftari Husna Bernard akipokea misaada hiyo kwa niaba ya wenzake
....Mmoja wawahanga hao akiangua kilio baada ya kuchomwa na maneno yaliyosema na mmoja wawahanga wenzake Husna Bernard
Kaimu mwenyekiti wa Tawi la Simba Samora Mwarabu naye akikabidhi Msaada wake kwa familia hizo
....Mzee Mwambeta ambaye ni mmoja wa viongzo wa Baraza la Wazee wa tawi la Simba naye akitoa msaada wake kwa familia hizo
Maafande wa Kikosi cha Zima Mato na Uokoaji Mkoa wa Morogoro wakizima Moto huo siku ya tukio Jumapili iliyopita.

 

 

 Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

Wanachama wa matawi Makuu ya Simba na Yanga Mkoa wa Morogoro juzi wameweka kando tofauti zao na kuunga pamoja kwenda kutoa msaada kwa kaya 9 zilizokosa makazi baada ya nyumba waliokuwa wakiishia  kuteketea kwa Moto wiki iliyopita..

 

Nyumba hiyo  iko  Mtaa wa Makaburi C kata ya Mji Mpya  jirani kabisa na ofisi kuu za matawi hayo ya Simba na Yanga yenye nguvu kubwa kwa timu hizo kongwe nchini zenye makao yake Makuu Jijini Dar es Salaam.

 

Wanachma hao  waliongozwa na wenye viti wao wa matawi  Mwenyekiti wa tawi la Yanga lssa Kitukwa Maarufu lssa Chabala na Mwenyekiti wa tawi kuu la Simba Said Mkwinda. ambao kwa pamoja walimkabidhi vifaa vya shule, kwa wanafunzi wa familia  hizo kwa  mmoja wa wahanga hao Husna Bernard

 

Wakizungumza na Mwandishi wa habari hizi wenyeviti hao wa matawi ambao pia ni wenyeviti wa serikali za Mitaa kwa leseni ya CCM  Issa Chabala mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Fumilwa A Kata ya Mji Mpya na Said Makwinda Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Simu C Kata hiyo hiyo ya Mji Mpya walisema wameondoa tofauti zao na kuungana kutoa Misaada kwa familia hizo.

 

“ Kama unavyofahamu Shekidele majirani zetu walipata majanga ya kuunguliwa na nyumba yao na kaya 9 zimeathirika na tukio hilo tunaamini kwenye familia hizo wapo mashabiki wa timu zetu za Yanga na Simba vile vile wahanga hao ni majirani zetu  kwa sababu hizo sisi viongozi wa matawi tumeketi kikao tukakubalia kuwashirikishe wanachama wetu kuchangia chochote kwa lengo la kuwapa misaada wenzetu hawa”walisema wenyeviti hao,

 

Kwa upande wao wahanga hao kupitia mwakilishi wao Husna Bernard wamewashukuru wanachama hao wa Simba na Yanga kwa Msaada huo.

 

” Tunashukuru sana kwa msaada ya madaftari kalamu na Soksi tunaamini kesho Vijana wetu watakwenda shule kwani toka tukio litokee hawajaenda shule baada ya madafutali yao na sale  zao shule kuteketea kwa Moto”alisema Husna na kuongeza kusema

 

” lngawa mpaka sasa hawana sale za shule watakweda shule na nguo za nyumbani mpaka tutakapopata wasamalia wengine wenye wa kusaidia sale hizo za shule,kikubwa wamepata Madaftari na kalamu kwani baadhi ya watoto wetu wako darasa la saba na mitihani ya taifa inakaribia hivyo kuendelea kukaa nyumbani wanapitwa na masomo”alimalizia kusema Husna kauli hiyo ilimzima mmoja waaanga hao kama anavyoonekana Pichani akifuta machozi.

 

 Nyumba hiyo iliteketea kwa Moto Jumapili iliyopita majira ya saa 12 jioni na kuteketeza nyumba hiyo iliyokuwa na nyumba 9 ambapo vifaa vyote vya wapangaji hao 9 ziliteketea kwa moto hali iliyosababisha kaya hizo 9 kuhifadhiwa kwa majirani nyakati za usiku na kwamba majira ya Mchana familia hizo zinashinda kwenye eneo la nyumba yao iliyoteketea kwa moto kwa lengo la kupokea pole na misaada kwa wasamalia wema. Mtandao huu unatoa wito kwa yoyote atakaye guswa na tukio hilo afike kwenye eneo hilo kuwaptia msaada familia hizo hasa chakula na sale za shule kwa wanafunzi wa familia hizo.

 

Kwa wale wageni eneo hilo alipotezi fika shule ya Msingi Mwembesongo kuna vijiwe vya boda boda mulize boda boda yoyote atakuonyesha eneo hilo kwa kile.

 

 

 

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...