Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Wednesday, September 28, 2022

WAZIRI WA ZANZIBAR JUZI AMEFUNGUA MASHINDANO YA BANDARI MOROGORO


Mkuu wa Wilaya wa Morogoro akiwasili Uwanja wa Jamhuri Morogoro
...Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo serikali ya Mapinduzi Zanzibar akiwasili uwanja wa Jamhuri Morogoro
Wafanyakazi wa Bandari na Maziwa wakiingia uwanja wa Jamhuri kwa maandamano yaliyoongozwa na Matarumbeta






Wanamichezo wa bandari waliofariki dunia kwa sababu mbali mbali
Kiongozi wa wamuzi Wilaya ya Morogoro Juma Simba akira Kiapo cha kutenda haki yeye na wamuzi wenzi kwenye mashindano hayo
Mkuu wa Wilaya ya Morogoro  Mh Albart Msando akizungumza kwenye uzinduzi huo
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bandari Tanzania Juma Kijafara
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro SACP Fortnatus Muslim

             Kundi la wanamichezo hayo wakizagaa uwanjani
.....Waziri Tabia na mwenyeji wake Msando wakielekea uwanjani kuzindua mashindando hayo
        Waziri Tabia Mwita akifungua mashindano hayo

 

Mzee wa Nyakua nyakua akiwa na Mwandishi wa Mtandao huu.

. Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

WAZIRI wa Habari,Vijana, Utamaduni, na Michezo kutoka Serikali ya Mapunzi ya Zanzibar Mh Tabia Mauli Mwita, juzi amefungua mashindano ya 16 ya Bandari na Mziwa Tanzania bara na Visiwani.

 

 Zawadi wa wafanyakazi mia 5 kutoka Bandari za Dar es salaam, Tanga, Mtwara na Zanzibar pamoja na Maziwa ya Victor, Nyassa na Tanganyika kutoka Mikoa ya Mwanza na Kigoma wanashiriki mashindano hayo yaliyoanza Septemba 26 na kutamatika Octobar 3.

 

Akizungumza kwenye ufunguzi wa mashindano hayo yanayofanyika katika Viwanja vya Jamhuri na Chuo Kikuu cha Kiislama Morogoro’MUM’ kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bandari Tanzania Juma Kijafara ameiomba serikali  mashindano hayo yafanyike mara 2 kwa mwaka tofauti na sasa ambapo yanafanyika mara 1 kwa Mwaka. Naye Waziri wa Tabia Mwita aliwaomba waandaji mwakani Mashindano hayo yafanyike kwenye visiwa vya karafuu Zanzibar huku akilipokea ombi la Viongozi hao kuomba mashindano hayo kufanyika mara kwa Mwaka.

 

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albeth Msando aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Mwassa aliwahakikishia usalama wanamichezo hao kwa siku 8 watakazokuwa mkoani Morogoro.

 

”RPC Musilim Mzee wa Nyakua nyakua yuko hapa anasikia ahadi hii hii, pia kwa Morogoro kuna vivutia vingi zikiwemo mbugha za wanyama hivyo mtakapopata nafasi tembeleeni vivutio hivyo” alisema Mkuu huyo wa Wilaya aliyetinga uwanjani hapo na suti ya kombati.

 

 Kabla ya Waziri huyo kuzindua mashindano hayo yanayofanyika kwa mara ya 5 mfurulizo Mkoani Morogoro,washiriki wote walisimama kwa dakika 1kuwaombea wanamichezo 2 waliofariki dunia siku kabla ya mashindano hayo kuanza

 

 Kama kawaida Mwandishi wa Mtandao huu umekusanya matukio kibao kwenye ufunguzi huo hivyo endelea kuwa jirani na Mtanda huu muda wote.

 

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...