Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Thursday, September 29, 2022

VIGOGO CCM NAO WATOA MSAADA KWA WAHANGA WA JANGA LA MOTO.


Vigogo wa CCM Kata ya Mji Mpya wakipozi mbele ya kamera za Mtandao huu kabla ya kukabidhi msaada kwa wahanga wa janga la Moro.
Kutoka kushoto waliosimama ni Katibu mkuu wa JWT Kata ya Mji Mpya Bi.Adella Mdede'Mrs Mlowa au Mwalimu Mlowa Chukia Abdallah Mjumbe wa halmashauri kuu JWT Kata. Kombo Nkumilwa Mwenyekiti wa CCM Kata.Melle Kunambi Katibu Mkuu wa CCM Kata.Seleman Kasanga Katibu Mwenezi Kata na Rehema Matonya Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa ngoma C Kata ya Mji Mpya.
Waliochutama kutoka kushoto ni Zaituni Rajabu Mwenyekiti Jumuiya ya Wazazi tawi la Ngoma na kulia ni Amir Benne Mhasibu Kata ya Mji mpya..






 


 

             Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

 

VIGOGO wa Chama Cha Mapinduzi’CCM’ Kata ya Mji Mpya Mkoani hapa.wiki iliyopita wametinga mtaa wa Makaburi C Kata ya Mji Mpya kuwapa pole Kata 9 zilizounguliwa na nyumba yao mwanzoni mwa mwezi huu.

 

Viongozi hao wa Chama tawara waliotinga kwenye eneo hilo ni pamoja na Mwenyekiti wa CCM Kata ya Mji Mpya Kombo Nkumilwa, Katibu Mkuu wa CCM Kata Melle Kunambi, Katibu Mwenyezi Kata Selemani Kasanga na Katibu wa JWT Kata Adelle Mdede’Mrs Mlowa Maarufu Mwalimu Mlowa.

 

Wengine ni Chukia Abdallah Mjumbe Halmashauri Kuu JWT Kata, Zaituni Rajab Mwenyekiti Jumuiya ya Wazazi tawi la Ngoma na Rehema Matonya Mwenyekiti Serikali ya Mtaa wa Ngoma C Kata ya Mji Mpya kwa leseni ya CCM.

Vigogo hao wa CCM Kata waliongozana na Afisa Mtendaji Tekla Mbaruko mwenye gauni la kitenge pichani na Mwandishi wa habari hizi.

 

 Kabla ya kumkaribisha Mkuu wa msafara huo kuzungumza na wahanga hao  Mwenyekiti wa CCM Kata, Katibu Mkuu CCM Kata Bi, Melle Kunambia aliwapa pole wahanga hao kwa janga hilo la Moto akisema CCM Kata ipo pamoja nao kwenyekiti hiki kigumu wanachopitia.

 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Kata Nkumilwa,mbali ya kuwapa pole kaya hizo 9 pia aliwapa kifuta jasho la shilingi laki moja kwa maana kila kaya  elfu 11.

 

”Mtakumbuka siku ya tukio Jumapili iliyopita wakati nyumba inaungua majira ya saa 12 jioni mimi nilikuwa hapa mpaka saa 5 usiku nikihakikisha kaya zote 9 mnapata sehemu ya kulala kwa usiku ule”alisema Mwenyekiti huyo  aliyeingia madarakani takribani miezi 2 iliyopita baada ya kuibuka kidede kwenye uchaguzi mkuu wa CCM Kata akimbwaga mpinzani wake mkubwa Said Kondo aliyekuwa akikalia kiti hicho. 

Mwanzoni mwa wiki hii Viongozi na Wanachama wa Matawi Makuu ya Simba na Yanga  Mkoani Morogoro yenye Maskani yao Kata hiyo ya Mji Mpya kwa pamoja waliweka kando tofauti zao wakaungana kutoa Msaada kwa kaya hizo 9.

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...