Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Tuesday, August 23, 2022

YA SARAMBA YA KUOMBA VIATU KWA MZUNGU YAMEJIRUDIA MORO

                Mchezaji wa Simba akimuomba Viatu Mzungu

 Mzunguyo akiwajibika uwanjani huku akiwa ametinga Viatu hivyo kabla ya kuvigawa na mchezaji wa Simba Under 20


.

                 Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

 

Mchezaji wa timu ya tawi kuu la Simba la Mkoani Morogoro  Shujaa Under 20 Denis Michael, amemuomba Viatu Mzungu Luia Friedrich raia wa Ujerumani mara baada ya kutamatika kwa mchezo wa kirafiki kati ya timu mbili za tawi hilo za Vijana chini ya miaka 20 na 17.

 

Gemu hiyo iliyopigwa  uwanja wa Shujaa uliopo Kata ya Mji Mpya Manispaa ya Morogoro unaomilikiwa na tawi hilo la Simba Maarufu tawi la Shujaa Ngome Kuu’Denis alimkimbilia mzungu huyo na kumuomba Viatu ambapo bila hiyana Mjerumani  huyo alimvulia viatu na kumkabidhi..

 

Hata hivyo kwa muonekano Viatu hivyo vilionekana kuwa vikubwa’Over Size’ kwa mchezo huyo kutokana na utofauti wa maumbile ya wawili hao.

Kufutia hali hiyo Mwandishi wa habari hizi alimfuata Denis na kuzungumza naye ambapo awari amekili kumuomba Viatu Mzungu huyo na alipoulizwa ukubwa wa Viatu hivyo alijibu.

 

” Ni kweli Jamaa Miguu yake ni mikubwa kuliko yangu kwa vile na mimi  bado na kua nitavitunza mpaka nitakapokuwa mtu mzima nitavivaa na kuvitumia kwenye michezo mbali mbali ”alisema Denis huku akiwa na furaha ya kupewa Viatu hivyo OG.

 

lkumbukwe miaka kadhaa iliyopita Simba ilicheza mchezo wa kirafiki na timu ya Sevilla inayoshiriki ligi kuu ya Hispania na ligi ya Mabingwa Ulaya.

 

Mara baada ya mchezo huo uliopigwa dimba la Mkapa jijini Dar kutamatika Mchezaji wa Simba Saramba alimkimbilia mchezaji mmoja wa Sevilla na kumuomba Viatu, ambapo mzungu huyo alivua viatu hivyo na kumkabidhi mchezaji huyo.

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...