Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Tuesday, August 23, 2022

LETE MZUNGU-LETE MZUNGU. MZUNGU MWINGINE WA SIMBA AFANYA BALAA KUBWA MOROGORO.

Mzungu wa Simba Moro Luia Friedrich[kulia] akigombea Mpira na beki Shariff Salum




.....Baada ya kufanikiwa kumpoka mpira beki huyo Mzungu akitoa basi ya bao kw amfungaji
.....Mfungaji akifunga bao baada ya kupeka pasi ya upendo kutoka kwa mzungu

 Friedrich akihojiwa na Mtandao huu,huku akiwa ametinga uzi wake wa Simba

       Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

Kwa sasa habari ya Mjini hasa  kwenye Mitandao ya Kijamii ni mchezaji mpya wa Simba Bejan Raia wa Sebria,baada ya kuzihakiwa na mashabiki wa timu pinza, wakidai mchezaji huyo hana uwezo wa kucheza soka na kwamba Simba wamepigwa kwenye usajiri wa mchezaji huyo.

 

Wanazi hao walifikia dhihaka hiyo  baada Mzungu huyo  kutofanya vizuri kwenye michezo miwili mmoja wa ligi kuu na ule wa kirafiki siku ya tamasha la Simba Day, juzi Mzungu huyo alikata ngebe na Viherehere vya mashabiki hao waliomdhihaki baada ya kufunga bao la kideo kwenye mchezo wa ligi kuu dhidi ya Kagera Sugar.

 

Baada ya Bejan kufunga bao hilo alikwenda kulishangilia jukwaani akiwasaka wale mashabiki  waliomdhihaki na kukata mauno kwa Style ya kucheza kale kamziki kao ka Lete mzungu Lete Mzungu akiwajibu kwamba amekuja sasa wana semaje.?.

 

Wakati hayo yakiendele huko jijini Dar,huku Morogoro’Mji Kasoro Bahari’ Mzungu Mwingine Luia Friedrich ameibuka akiitumika timu ya Simba B inayomilikiwa na tawi kuu la Simba Mkoani Morogoro.

 

Friedrich raia wa Ujerumani ambaye yeye na familia yake ni marafiki wa tawi hilo, Maarufu tawi la Shujaa Ngome Kuu wiki iliyopita aliitumikia timu ya Shujaa Under 20 kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya timu C ya Shujaa Under 17.

 

Katika mchezo huo wa kirafiki uliopigwa  Uwanja wa Shujaa uliopo Kata ya Mji Mpya Morogoro timu hizo zilitoka sale ya bao 1-1 huku Mzungu huyo wa Simba Morogoro aking’ara kwenye mchezo huo huku akito basi ya bao’Assit’baada ya kumtoka kwa kasi beki wa Shujaa Under 17 Shariff Salum na mzungu huyo akampenyezea pasi ya Upendo mfugaji wa bao hilo la kusawazisha.

 

Cheki Picha za tukio hilo Mzungu huyo akimchekeza beki huyo, ifahamike Vijana hao wa Shujaa wenye umri chini ya 20 na 17 wanapoonyesha viwango vya juu hupelekwa timu ya Simba B ya jijini Dar na baadae kupandishwa hadi timu wa wakubwa Simba inayoshika nafasi ya 14 kwenye viwango wa CAF.

 

lkumbukwe kwenye ramani ya dunia bara la Afrika  ndio bara kubwa duniani likiwa na nchi 54 na timu zaidi ya lakini,  kupitia takwimu za Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika’CAF’za mwaka huu zinaonyesha Simba inashika nafasi ya 14 kwa ubora barani Afrika.      

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...