Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Saturday, August 27, 2022

SEHEMU YA PILI STORI BODA BODA KUDAIWA KUFUMANIWA NA DADA WA KAZI.


 


          Na Mdakuzi Dunstan Shekidele.Morogoro.

 

 STORI hii ya fumani ya boda boda kudaiwa kufumaniwa na dada wa Kazi chumbani kwa bosi wake Kihonda Maghorofani Mkoani hapa,ilianza kuripotiwa jana kwenye Mtandao Pendwa wa Shekidele.

 

Stori hiyo iliishia sehemu tamu ya Mmiliki wa nyumba hiyo Mwanadada Mrembo kutonywa na Majirani zake na kuludi fasta nyumbani akitokea kazini kwa lengo la kuwafumani Wapenzi hao waliogeuza ‘geto’ nyumba yake alipofika hapo nini kiliendelea  twende pamoja kumalizia stori hii.

 

Mrembo huyo baada ya kufika nyumbani akiwa na gari lake la kisasa nje ya Mjengo wake wa kifahari alikuta boda boda mpya imepack alishuka kwenye ndinga yake  kazama ndani kwa lengo la kuwafumania wapenzi hao kwa lengo la kukomesha mchezo huo mchafu unaofanyika nyumbani kwake bila ridhaa yake. 

 

Dili limebuma House Girl huyo baada ya kusikia mngurumo wa gari la bosi wake ambao kimsingi anaufahamu vizuri, fasta kumfungulia boda boda huyo mlango wa nyuma,katimua mbio kama zile za swala anayekimbizwa na chita’Chui’kaiacha boda boda yake pamoja na kofia ngumu’Herment’ kwenye moja ya Masofa yaliyopo kwenye sebreni ya Mjengo huo.

 

Mmiliki wa  nyumba hiyo zlipzama ndani alianza kumtafuta boda boda huyo maeneo yote ya nyumba hiyo bila mafanikio,  alipoingia chumbani alikuta shuka za kitandani zimekunyamana kama vile zilitafunwa na Ng’ombe kisha zikatemwa.

 

Big boss huyo wa Mjengo huyo baada ya kumkosa boda boda huyo alimvaa house girl, alipoulizwa alikosa majibu sahihi kutokana na ushahidi wa Pikipiki, Herment na kule chumbani ushahidi wa kuvulugika kwa akitanda kwa ushahidi huo dada huyo wa kazi hakuwa na jibu lingine  zaidi ya kukubali kosa na kumuomba msamaha bosi wake.

 

House Girl huyo baada ya kukubali kosa hilo la kumwingiza boda boda chumbani na kushirikiana naye kuivunja amri ya 6 ya Mwenyezi Mungu ya Usizini,Mmiliki huyo wa mjengo aliamua kuichukua boda boda hiyo na kuifungia ndani akihitaji kulipwa kiasi cha pesa akidai  kwa  siku nyingi vitu vyake zilikuwa vikiibiwa ndani kwa ushahidi huo anaamini mwizi wake ni boda boda huyo hivyo kamua kuikamata Pikipiki hiyo mpaka alipwe laki tano.

 

Uchunguzi wa awari uliofanywa na Mdakuzi ulibaini boda boda huyo alipewa Pikipiki hiyo na bosi wake kwa mkataba wa kila siku kukusanya elfu 10 na pesa hiyo walikubaliana kuikabidhi kwa wiki elfu 70.

 

Utamu unakuja hadi jana ljumaa habari hii inakwenda hewani ni takribani siku 5 hivyo bado siku 2 boda boda huyo kuhitajika kupeleka kipande cha elfu 70 kwa tajiri yake huku boda boda hiyo iking’ang’aniwa na ‘Mother House’ huyo.

 

 Baadhi ya marafiki wa boda boda huyo walimshauri amtafute Mzee mwenye busara  waendele kwa Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa lilipotokea tukio hilo wakamuombe Msamaha dada huyo ili amludishie  Pikipiki yake aendelee na ajira yake.

 

lnadaiwa boda boda huyo mwenye jina la Moja ya Mikoa ya Kanda ya Ziwa anaogopa kufanya hivyo akihisia majanga yanaweza kuwa makubwa zaidi akihofia huenda akakamatwa na kupelekwa Polisi.

 

Maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani’Mei Mosi’ yaliyofanyika kitaifa jijini Dodoma Mwaka huu  Mh Rais Samia Suluhu Hassan kwenye hotuba yake alisema Wafanyakazi wa ndani wanahaki kama wafanyakazi wengine.

 

Wakistahili kupata huduma zote kama wafanyakazi wengine ikiwemo yakuutengewa chumbani na bosi wake endapo akitokea house Girl akipata mchumba aweze kuishi naye  kwenye nyumba hiyo  bila bughoza yoyote.

 

 Kauli hiyo ya Mpendwa Rais wetu Mama Samia iliyobeba zana kuu ya kuwatetea wafanyakazi hao wa ndani, iliamsha vicheko kwa umati wawatu waliokuwepo kwenye mkutano huo na wale waliokuwa wakimfuatilia  kupitia Luninga.

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...