Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Saturday, August 27, 2022

UJUMBE WA NENO LA MUNGU WANADAMU WENGI WANAPOTAKA KUONA AU KUOLEWA WANATANGULIZA TAMAA MBELE.


 


 

MITHALI 31-10.

 

 “Mke Mwema ni Nani awezaye kumwona? Maana Kima Chake Cha Pita Kima Cha Marijani”

 

1.SAMWELI .16-7.

 

”Lakini Bwana akamwambia Samweli,Usimtazame Uso wake,wala urefu wa Kimo Chake,Kwa Maana Mimi nimemkataa,Bwana hangalii Kama binadamu aangaliavyo,Maana binadamu utazama sura ya nje, bali Bwana hutazama  Moyo.”

 

Somo letu la leo Jumapili ya Mwisho ya Mwezi wa 8 linatuongoza kumjua  Mke au Mume Mwema.

 

Baadhi ya wanadamu wa kizazi hiki cha kidigital cha kuanzia miaka ya 80 mpaka 2022 tunapoingia kwenye mchakato wa kutafuta mke au mume tunavipa kipaumbele vigezo vya matamanio ya nje na si ya ndani Kwa maana ya Moyo na tabia njema za mtu.

Wanandoa hao wanapotaka kuingia kwenye ndoa hutafuna hutangulia tama za Mwili na Mali,kama vile  Shepu, Sura,Mali, Madaraka au Cheo, huku tukikipa kisogo kigezo Mama cha moyo safi na tabia njema.

 

 Hali hiyo ndiyo inayotajwa kuwa chanzo cha ndoa nyingi cha kizazi hicho cha kutoka miaka ya 80 mpaka mwaka huu 2022 tofauti na ndoa za wazee wetu ambao ndoza zao hudumu mpaka mmoja wao anapotangulia mbele za haki’wanazikana’.

 

Kuna siku nilistuka sana baada ya kusikia taasisi moja ikitoa takwimu kwamba kwa mwaka jana pekee talaka mia tano[500] zimetolewa kwa maana ndoa 500 zimevunjika.

 

 lkumbukwe kuna dini nyingine ndoa zao zikifungwa hakuna kipengere cha kupeana taraka sasa huenda idadi hiyo ya taraka 500 ndoa hizo hazijajumuishwa ingawa huko Mtaani tunashuhudia  wanandoa hao wengi wao wameshabwagana kitambo.

 

 Kwa sasa wanaume wengi  wanapotaka kuoa wanatafuta mwanamke mrembo mwenye shepu, rangi iliyokorea wengine wanafika mbali zaidi wanasaka mwanamke mwenye jina kubwa mjini ili naweze kuwatambia marafiki zake kwamba ameoa mwanamke Super Star Mjini.

 

Hali kama hiyo pia iko kwa wanawake,  wao vigevyo vyoa vikuu ni kutafuta mwanaume mwenye Pesa, au Mali Kwa maana ya nyumba na Magari hawaangalia tabia njema na moyo safi wa mwanaume atakaye kuwa baba bora wa watoto zake au Mama bora wa familia yako.

 

lnafaida gain unaolewa na mwanaume mwenye Pesa na Mali mwisho wa siku anakuwa sio baba bora wa watoto wako kila siku anarejea nyumbani 8 usiku akiwa amerewa.

 

Hana hata muda wa kuketi na familia yake kupanga Maisha  nyakati za jioni baada ya kumaliza kazi.

 

Mwisho wa siku huyo mwanaume akifirisika ndoa inavunjika kwa sababu ulichofuata hakipo tena,.

 

 Hakika ukitafuta mwanaume mwenye tabia njema na moyo safi hutakumbana na kadhia hiyo kila siku ndoa yenu itakuwa mpya.

 

Najua kwenye ndoa sio peponi kwamba ukiingia utakutana na furaha ya Milele hapana,kuna changamoto zake kwa sababu binadamu sio mkamilifu kama Malaika, hivyo nawasihi na kuisihi nafsi yangu tubebeane Misalama ya changamoto zetu ili tufike kwenye ile nchi ya ahadi tunayoitamani.

 

Kwa kizasi hiki cha kuanzia miaka hiyo ya 80-2022 natoa Kongore kwa wanandoa wote ambao mpaka sasa ndoa yao inaumri wa kuanzia miaka 5 na kuendelea hongereni sana na Mungu aendelee kuibariki ndoa hiyo.

 Ushauri kwa wale wanaohitaji kuingia kwenye ndoa na wale wanaohitaji kuinge  tena kwenye ndoa  baada  ya ndoa zao za awari kuvunjika kwa  kamwe usimtafute mwenzi wako kwa tama za Sura, Shepu au Mali mshirikishe Mungu na kigezo chako kiwemo tabia njema na Moyo safi mwengine yatapatikana kwa juhudi zenu kwenye mipango yenu ya kimaisha.

 

Kwa leo mtumishi wako naishia hapa tukutane Jumapili ijayo kwa uchambuzi mwingine wa neno la Mungu.

Amani ya Mwenyezi Mungu na iwe Juu yenu wote tuseme Amen’

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...