Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Sunday, August 21, 2022

UTOAJIA WATOTO KAFARA,UPIGAJI RAMLI NA UCHAWI VYOTE HIVYO VIMEKATAZWA NA MUNGU.


Majira ya saa 1 kasoro usiku mwenzi ukichomoza eneo la Milima ya Uluguru

Mwandishi wa Mtandao akiw akileleni kabisa mwa Milima ya Uluguru
Muonekna wa Mji wa Morogoro baada ya Mpiga Picha wa Mtandao huu kupiga Picha hii akiwa keleleni kabisa mwa Milima ya Uluguru eneo la Morning Site Kata ya Mlimani Manispaa ya Morogoro

 Mwandishi wa Mtaa huu akiwa juu ya Milima ya Uluguru eneo la Mgeta Wilaya ya Movome
 

 

KATAZO HILO LINATOKA KUMBUKUMBU YA TORATI SURA 18 -9-14.

”Utakapokwenda kuingia katika nchini,akupayo Bwana Mungu wako usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya Mataifa yale.

Asionekane kwako mtu ampitishaye Mwanawe au binti yake kati ya Moto, wala asionekane mtu atazamaye bao,wala mtu atazamaye nyakati mbaya,wala mwenye kubashiri wala msihiri.

 

 Wala mtu alogaye kwa kupiga Mafundo,wala mtu awaombeaye wafu.

 

Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana Mungu wako anawafukuza mbele yako.

 

Uwe mkamilifu kwa Bwana Mungu wako.Maana Mataifa haya utakaowamiliki huwasikiliza wanaoshika nyakati mbaya na kutazama bao,bali wewe Bwana Mungu wako hakukupa ruhusa  kutenda hayo” Hilo ndilo neno letu la leo Jumapili ya Agost 21.

                      UCHAMBUZI.

Nakumbuka kuna siku nilikwenda kushiriki msiba wa Mzee mmoja Maarufu mkoani Morogoro ambaye ni Mluguru, kwenye lbada ya msiba huo uliofanyika nyumbani kwa marehemu Kigurunyembe Mizambarauni Padre aliyeongoza lbada hiyo alikuwa  pia ni Mluguru na alipotupa jicho kwa waombolezaji alibaini wengi wao ni Waluguru.hivyo  Kwenye mahubiri yake kuna sehemu aliweka msisitizo kwa kutumia lugha ya Kiluguru.

 

” Kwa sasa kuna baadhi ya familia mtu akifariki hata kwa ajari ya gari wao hawaamini kama kafa kwa agizo la  Mungu kwa kina nafsi itaonja umauti, wao wana kwenda kupiga bao kuangalia nini kimemuua ndugu yao.

 

Baadhi ya Waluguru wenzangu  tabia hiyo tunayo utasikia familia iliyofiwa ikisema kwa Kiluguru [Chimkomile Choni?] Yaani nini kimemuua? Basi hapo familia itachanga pesa kwenda kwa Mganga kupiga bao kupata majibu la kichomuua ndugu yao.

 

Majibu hayo ni uchonganishi Mtupu, utaambiwa marehemu wenu amerogwa na yule mzee mwenyekipata pale mtaani kwenu.

 

Mnajifunga kibwembwe kwenda kugombana na huyo mzee wa watu mwisho wa siku mnajikuta mkiongeza matatizo kwa kukamatwa na Polisi”alisema Padre huyo na kupokea zawadi ya makofi mawili matatu kutoka kwa waombolezaji.

 

Naamini Padre huyo aliyasema hayo akinukua maneno haya kutoka kwenye Biblia, Somo hili linakemea uchowi na ushirikina na kutegemea nguvu za binadamu huku ukimpa kisogo Mungu.

 

Baadhi ya mambo ya kuliyokatazwa na Mungu kwenye neno hilo ni Pamoja na kupiga Ramli, kuvaa hirizi’hapo wamesema fundo na kubashiri wale mashabiki wa soka wanao Bet mjuwe  kufanya hivyo ni chukizo kwa Mungu. Kwa leo mtumishi wako naishi hapa Mungu akipenda tukutane Jumapili ijayo endelea kuwa jirani na Mtandao huu siku zote.

                        


                               

                              

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...