Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Tuesday, April 5, 2022

YARIYOJILI KUMBI ZA STAREHE MWISHONI MWA WIKI. MAISHA MAPYA YASAJILI WANENGUAJI WAPYA.

Menguaji Mwenyeji Husna Ramadhan kushoto akiongoza utambulishwa wawanenguaji Wapya wa band hiyo Kavela’Kati’ na Hamida Kulia

Maisha Mapya

“Mimi sio mkali wa kuosha mafuso Tu hata kusakata Sebene najua'

Ndivyo anavyoonekana kusema Muosha Magari Maarufu Mkoani Morogoro Jangara wa Kilosa. anayepiga kazi kando kando ya Mto Morogoro daraja la Shani Sinema akionyesha umahiri wake wa kusakata Sebena akishindano ya wanenguaji wa band Maisha Mapya

Husna Ramadhan akizidi kuuwasha Moto 5 Mnenguaji Mahiri wa band ya Maisha Mpaya Husna Ramadhan ambaye mwaka jana akiwa na Marehem Tatu walijiunga na band ya Maisha Mapya wakitokea FM Academia ya jijini Dar akiwajibika jukwaani wiki end iliyopita.

Picha ya chini

 



 

Mnenguaji ingizo Jipya wa band ya Maisha Mapya Kavera a.k.a No ya Siri akiuwasha Moto wakati alipotambulishwa kwa mara ya kwanza na band ya Maisha Mpya


            Na  Mlala Nje Dunstan Shekidele,Morogoro.

BAADA ya kufiwa na Menguaji wake Mahiri siku za hivi karibuni Marehemu Tatu, bendi Pendwa ya Maisha Mapya wikiend iliyopita imetambulisha wamenguaji wawili  kutoka jijini Dar es salaam.

 

Wanenguaji hao wakali wa kukata ‘nyonga’ ni Mwanadada Hamida a.k.a Mama Segele na Mkaka Kavela a.k.a No ya Siri utambulisho huo umefanyika alhamisi iliyopita ndani ya Ukumbi wa JKT Bwalo la Umwema uliopo jirani na Uwanja wa Jamhuri.

 

Utambulisho huo ulishuhuidiwa na Mwanamuziki Mkongwe nchini Muumini Mwijuma ‘Kocha wa Dunia’ ambaye pamoja na Mambo mengine amesifu uwezo mkubwa wa wasanii wa band hiyo ya Maisha Mapya.

 

”Morogoro kuna Vipaji vya kila aina ama kwa hakika band hii ya Maisha Mapya inawanamuziki wenye Vipaji vikubwa sana hasa huyu dogo anayepiga gitaa la Solo amenivutia mno”alisema Mwijuma huku akimshika bega mpiga gitaa huyo anayekadiliwa kuwa na umri wa miaka 20.

                  

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...