Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Thursday, January 27, 2022

GARI LASAFIRISHWA KWENYE MKOKOTENE.


 


 Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

Mwenyendesha Mkokotene alinaswa hivi karibuni alisafirisha gari bovu kutoka kwenye Magereji yaliyopo maeneo ya barabara ya Tumbaku akilipeleka kata ya Mji Mpya Mkoani hapa, kwa lengo la kwenda kuuzwa kama Chuma Chakavu.

 

Kuna taarifa zinadai kwamba kufuatia kukidhiri kwa wizi wa mara kwa Mara kwenye Miundombinu ya serikali, Kama Vile alama za barabaranai, Kingo za Madaraja,na Taa za barabarani.biashara ya Vyuma chakavu imepigwa marufuku kwa lengo la kulinda Miundombinu hiyo.

Siku za hivi karibuni Vibaka walivamia nyumbani kwa Mlemavu Mtaa wa River Side Kata ya Mwembesongo Majira ya Usiku na kuiba baiskeli yake ya mataili 3.   Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi Mlemavu huyo wa Miguu [jina linahifadhiwa kwa sababu za kiuwanaume]alisema.

 

”Kama unavyoona Mlango wa chumba changu ninachoishi na mke wangu ni Mwembemba baiskeli  haikuweza kupita hivyo Miaka yote nilikuwa nailaza hapa nje ya Mlango wa chumba changu”alisema Mlemavu huyo na kuongeza.

 

 “Nyumba hii haina uzio iko wazi Jamaa wamekuja usiku wameichukua baiskeli yangu wameenda hapo Mtoni wakaikata kata na msumeno wakaenda kuuza Vyuma Chakavu kulipokucha nilipofungua Mlango sikuiona baiskeli Majirani wakaniambia walipoenda kuchota Maji mtoni wameona mabaki ya vyuma eneo hilo la Mtoni ndio hivyo tena wamechukua miguu yangu kwa sasa niko tu ndani sitembei ndio Maana hunioni Mjini”alisema Mlemavu huyo.

 

Kufutaia hali hiyo Mwandishi wa Mtandao huu aliguswa na kuamua kuendesha harambee kwenye Mtandao huu na kufanikiiwa kupata pesa za kumnunulia  baiskeli nyingine ingawa ilikuwa imetumika.

Mtandao huu unawashukuru wote waliojitolea kufanikisha zoezi hilo, Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema atawalipa Mara dufu pale mlipopunguza.

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...