Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Thursday, November 25, 2021

KUMBUKIZI YA MIAKA 5 YA KIFO CHA WAKALLA MAARUFU WA GLOBAL PUBLISHERS.

                     Marehemu Nasibu enzi za Uhai wake
Meneja Mkuu wa Global Abdallah Mrisho akizungumza kwenye mziba huo
Meneja Masoko wa Global Kivea akizungumza mbele ya jenera lililobeba mwili wa Marehemu
Vigogo hao wa Global waliofunga safari kutoka Dar Mpaka Moro kushiriki mazishi hayo wakiingia kwenye Noa yao wakirejea Dar
Kutoka Kushoto ni Laurence Kapande Mhasibu Mkuu wa Kampuni ya Global, Siafael Paulo Mhariri Mkuu wa gazeti la Ijumaa wikienda, Oscar Ndauka Mhariri Mtendaji Global na Abdallah Mrisho Meneja Mkuu Global Publishers
Mh Abbdas Mtemvu aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Temeke Dar

                                           Hussein Ngurungu


Na Dunstan Shekidele,Morogoro.  Novembar 25 -2016 aliyekuwa wakalla Maarufu wa Magazeti ya Kampuni Pendwa ya Global Pubrishers Mkoani Morogoro Nassib Nassoro alifariki dunia.

 

Hivyo jana November 25 2021 Mpendwa wetu huyo ametimiza miaka 5 toka alivyoiaga dunia. 

 

Hayati Nassib ambaye pia alikuwa Mhasibu Mkuu wa Msikiti Mkuu wa ljumaa wa Kata ya Mwembesongo na Mjumbe wa kamati ya Ujenzi wa shule ya Msingi na Sekondari inayomilikiwa na Msikiti huo alizikwa katika Makaburi  ya Familia yao yaliyopo Kingolwira Manispaa ya Morogoro.

Kwenye Mazishi hayo watu wengi maarufu walishiriki akiwemo aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Temeke  Mh Abas Mtemvu, Mchezaji wa zamani wa Pan Afrika Hussein Ngurungu ambaye rekodi yake ya kuitumika timu ya taifa ya Tanzania’Taifa Star’ kwa miaka 10 mfurulizo haijavunjwa na mchezaji yoyote mpaka sasa.  

Tutakukumbuka daima Mpendwa wetu Nassib Mungu akupunguzie adhabu ya kabri na akupokee na kukuweka unapostahiri kulingana na maisha uliyoishi hapa ulimwengungu.

 

                         

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...