Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Thursday, November 25, 2021

BABA NA MWANA WASHINDWA KUINUSURU TIMU YAO KUSHUKA DARAJA.

Yohana Semkia kushoto akitoa maelekezo kwa wachezaji wa Pam Fc. Kulia ni kocha kuu wa timu hiyo Lulusi  Yohana Semkiwa



 

 


Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

BEKI Kisiki wa zamani wa timu ya Reli ya Morogoro’Kiboko ya Vigogo’ Yohana Semkiwa’Mgosi’ wiki iliyopita aliradhimika kuacha shughuri zake binafsi na kumsaidia Mtoto wake Lulusi Semkiwa kuinusuru timu  ya Pam Fc isishuke daraja.

 

Lilusi ni kocha Mkuu wa timu ya Pam Fc iliyoshiriki ligi daraja la Tatu Mkoa wa Morogoro na kujikuta ikifanya vibaya na kuangukia kwenye Play Off ya kupigania kutoshuka daraja.

 

Timu nyingine zilizoangukia  Play Off ni Eleven Killer na New Kings, huku timu za Mkundi United, Kihonda United, Moro Youths.

 

Tanzanite Academy,Lukobe Fc na Mgude Worries zenyewe zikisonga hatua inayofuata kungana na timu kutoka vituo vingine,timu za Kihonda Maghorofani. John  Bosco na Kinonko zewenye zikisubiri msimu ujao.

 

Toka mashindano hayo yalipoanza mwanzoni mwa mwezi huu Uwanja wa Saba Saba kituo cha Morogoro Mjini, Mwandishi wa Mtandao huu alihudhuria michuano hiyo na hajawahi kumuona Yohaya Semkia uwajani hapo.

 Majuzi ndipo alipomuona kwenye hatua ya Play Off akiwa kwenye benchi la Pam Fc iliyokipiga na New Kings akiwa bize kutoa maelekezo kwa wachezaji na mwisho wa mchezo huu Pam alinyukwa bao 2-1.

Wachambuzi wa Mambo walisikika wakisema Semkiwa aliamua kumsapoti Mtoto wake kuliokoa Jahazi la Pam lisizame.

 

Hata hivyo licha ya Mzee Semkiwa Kumsapote Mwanaye lakini bado timu hiyo ya Pam yenye Maskani yake Kata ya Kichangani iliendelea kufanya vibaya kwa kufungwa michezo yote 2 ya Play Off na kujikuta ikikata tiketi ya kuelekea ligi daraja la Nne msimu ujao.

 

Mara baa ya  timu hiyo kushuka daraja Mwandishi wa Mtandao huu alimfuta Mzee Semkiwa na alipohojiwa alikiri kufika kwenye michezo hiyo 2 ya Play Off kwa lengo la kumsapoti Mtoto wake.

”Mgos Shekidele ni kweli nimeonekana kwenye michezo hii ya Play Off lengo kuu ni kumsaidi Mtoto wangu ili timu yake isishuke daraja lakini kwa bahati mbaya licha ya kucheza vizuri kwenye michezo yote 2  bahati haikuwa yetu tumefungwa na kushuka daraja”alisema Semkiwa ambaye alikuwa beki wa kulia wa Reli ya Morogoro.

Alipoulizwa mtoto wake huyo ni wangapi kwenye uzao wake alisema ni  wanne akitanguliwa na wakubwa zake 3.

 

Kwa Mijibu wa taarifa zilizopo kwenye Group la Chama Cha Soka Wilaya ya Morogoro ambalo Mwandishi wa Mtandao huu yumo,Kupitia Viongozi wa Chama Cha Soka Mkoa wa Morogoro kwenye ligi hiyo timu moja ya mwisho kwenye Play Off itashuka daraja hivyo baada ya michezo hiyo ya Play Off kutamatika jana kwa Pam kufungwa na Eleven Killer ni rasm timu hiyo imeshuka daraja.

                    

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...