Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Friday, October 15, 2021

NYERERE DAY 2021, MWANDISHI WA HABARI AMUENZI BABA WA TAIFA KWA KUENDESHA BAISKELI

Raiis wa kwanza wa taifa la Tanzania hayati Julius Kambarage Nyerere alipenderea kuendesha baiskeli enzi za uhai wake. 

 Mwandishi wa Mtandao huu naye mara kwa mara anapenderea kuendesha baiskeli ikiwa ni njia moja  wapo ya kumuenzi baba wa taifa

 Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

KUMBUKIZI ya miaka 22 ya kifo cha baba wa Taifa la watanzania,Mwl Julius Kambarage Nyerere.

Kila mtu anamuenzi kwa Style yake wengine kucheza bao wengine kukimbia na wengine kuiga sauti yake.

 

Kwa upande wangu namunzi kwa  kutembelea baiskeli kama alivyowahi kufanya yeye enzi za uhai wake licha ya kuwa na madaraka makubwa nchini rais laiki bado alitembelea na usafiri wa baiskeli ikiwa ni njia moja wapo ya yeye kufanya mazoezi ya utimamu wa mwili.

 

Rais huyo wa awamu ya kwanza alizaliwa Mwaka 1922 na kufariki dunia  14 Actobar 1999,hivyo kutokana na mchango wake uliotukuka kwa taifa hili imeamuliwa kila mwaka Octabar 14 inakuwa siku ya kitaifa ya kumbukizi ya Mpendwa wetu huyo na siku hiyo pia imeamuliwa kuwa siku ya wapunziko kwa taifa zima la Tanzania. 

Mtandao huu unasoma na watu wengi pande zote za dunia nakumbusha hapo juu kulia kuna sehemu ya kuchangua lugha chagua lughu yoyote usome habari zote zinazoruka kwenye Mtandao huu.kwa lugha unayoijua vizuri mpka lugha ya Kichina ipo


No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...