Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Saturday, September 18, 2021

WASIMAMIZI 6 WA MITHIHANI WAMEDAKWA NA POLISI WAKIJARIBU KUVUJISHA MAJIBU KWA MADENT



 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro akizungumza na Waandishi wa habari jana, mwandishi wa Mtandao huu mwenye nguo nyekuwa naye akiwa bize kukusanya matukio kwenye Press hiyo     

.

 

Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

 

JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro linawahojiwa wasimamizi 6 wa Mithihani ya darasa la 7 kwa madai ya kutaka kuvujishi Mithihani hiyo kwa wanafunzi waliofanya mithihani hiyo kote nchini Septemba 8 na kumaliza Septemba 9.

 

Tukio hilo limetokea   shule ya Msingi Kamhara iliyopo Wilaya ya Mvomero Mkoani hapa, ambapo wasimamizi hao kutoka maeneo mbali mbali ya Mkoa wa Morogoro wakipangiwa kusimamia kituo hicho.

Akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro SACP Fortunatus Musilimu amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

 

Amewataja wasimamizi hao kuwa ni Mwalimu Mkuu wa  Shule hiyo Juliana Thomas Nyumayo Kabira Mngoni mkazi wa Kamhara.

 

Msimamizi Mkuu wa Mithihani Anthonia Pastory Mchaga Makazi wa Doma Wilaya ya Mvomero, Msimamizi Mkondo  C  Francis Kondo Kabila Mkwere Mkazi wa Mkundi Manispaa ya Morogoro na Msimamizi Mkondo A Mwalimu Dorine  James Kiwia Mchaga Mkazi wa Madizini Tarafa ya Turiani Mvomero.

 

Wengine ni  Msimamizi Msaidizi B  Habibu Hango Mohamed Mwalimu wa Shule ya Msingi Mhonda Mnyiramba Mkazi wa Mhonda Turiani, wa Mwisho ni Mlinzi wa Mithihani kituo hicho cha MG Mohamed Bakuja Koila Mmasai Mlinzi Mfugaji Mkazi wa Kamhara.

 

”Kuna baadhi ya wanafunzi waliamini uwezo wao ni mdogo hivyo wahusika waliahidiwa pesa kwa lengo la kuwasaidi majibu ambapo watuhumiwa hao walipiga Picha kwa simu zao mithihani hiyo na baadae kuingia kwenye chumba cha Mthihani kuwapa majibu wanafunzi hao.

 Kwa vile Jeshi la Polisi tuliimalisha  ulinzi mkali tulifanikiwa kuwakamata wahusika kabla ya kuvujisha Mithihani hiyo na tunaendelea kuwa hoji uchunguzi ukikamilika tutawafikisha mahakamani”alisema Big bosi huyo wa Jeshi la Polisi ,Mkoa wa Morogoro. Baadae Mtandao huu utarusha habari ya Raia wa Canada kukamatwa na Silaha 3  hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu mufa wote                                


                                        

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...