Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Tuesday, July 6, 2021

HARUSI YA NURSE NA DEREVA WA DALADALA YATIKISA MOROGORO.

 


                       
Maharusi wakitoka ukumbini huku wakimbungiana Mikono na        wageni waalikwa baada ya hafra hiyo kabambe kukamilika

.........Wakipiga Picha na familia
.....Bwana harusi akiwapa zawadi ya saa wazazi wake
.......Bi harusi akiwapa zawadi ya Vitenge wakwe zake waliomzalia chema
......Mzazi wa bwana harusi akikabidhiwa benesi la nguo na vyombo

...Bwana harusi akimtunia Msanii wa nyimbo za lnjiri Chiba Son
.......Mahaba niuhee 'Nilishe ni kulishe ni lshara ya Upendo'


.......Maharusi wakishiriki kuimba na kwaya ya Kanisa la Sabato Misufini
.....Maharusi wakikaribishwa kinywaji baada ya kuketi kwenye viti vyao vya enzi
.....Bwana harusi akicheza wimbo wa kipare na shemeji zake
......Wakirishana keki yao ya harusi


 Baba Mchungaji Kachua Heliamani na Mkewe wakifuatilia kwa umakini harusi hiyo yab waumini wao
Baadhi ya Madereva wa daladala za Bingwa, Kihonda,  Dumila Mkundi, Lukobe, Mazimbu na Mikese wakimbeba juu juu dereva mwenzao wakimpongea kwa kufunga ndoa
Bi harusi akimtamburisha Mtoto wake ambaye alikuwa ni mmoja wa wahudumu kwenye harusi hiyo
....Maharusi wakiwatambulisha ndugu zao


,,,,Mc Oscar akifanya yake kwenye harusi hiyo
...Bi Harusi akiingia ukumbini



                         Na Dunstan Shekidele,Morogoro.
 
Bw Emmanuel Eliniak ambaye ni dereva wa daladala za Dumila- Mjini na Bi Zaina Vuliva ambaye ni Muuguzi ’Nurse’ wa Agape Adiventest Premary School, wamejiondoa kwenye timu dhaifu ya Ukapera a.k.a Usela na kujiunga na timu kabambe ya Wana ndoa inayokubarika duniani na Mbinguni. 
 
Wanandoa hao walipasha Moto Kiporo chao hivi karibuni, jana walifanya hafra kabambe iliyofanyika Ukumbi wa Mango Garden Uliopo Pande za Nungu Manispaa ya Morogoro. 
 
Katika sherehe hiyo iliyoratibiwa kisomi na kuongozwa na lmani ya dini ya Kikristo dhehebu la Sabato, watu walikunywa, Kula na kucheza Muziki Mwanzo Mwisho huku wanakwaya kutoka kanisa la Sabato Misufini wakiongozwa na maharusi pamoja na Mwimbaji binafsi Chiba Son walinogesha sherehe hiyo kwa kutoa burudani kali.
 
Vile vile nyimbo za asili za kabira la Kipare zilipata nafasi ya kuchezwa kwenye ukumbi huo, lfahamike Bwana harusi na Bibi harusi wote ni Wapare kutoka Mkoa wa Kilimanjaro. 
 
Katika sherehe hiyo Mpiga Picha wa Mtandao huu alibahatika kukutana na Mchungaji Kachua Heliamani anayeongoza kanisa la Sabato Misufini, Mtumishi huyo takribani miaka 10 iliyopita alimfanyia jambo Mpiga Picha wa Mtandao huu jambo hilo ambalo liligeuka kuwa la kuhudhunisha na baadae likageuka kuwa la kufurahisha, kisa hicho nitakurusha hewani hivi punde.
 
Kama kawaida Mpiga Picha Maarufu wa Mtandao huu ambaye pia ni ‘Photo Journalist’ndiye aliyepewa tenda na Kamati ya Maandalizi kupiga Picha Mtukio yote ya sherehe hiyo ya Kijanja. 
 
Kwa yoyote nayehitaji huduma ya Kupiga Picha bora za Kiwango zaidi ya cha lami kwenye shughuri yake awasiliane na Mpiga Picha wa Mtandao huu anayemiliki Kamera za Kisasa kwa namba 0627 48 80 20 namba ya Watsap 0715 28 90 73. 
 
Bei zake ni nafuu sana pia anatoa ofa kama vile Albam na kurusha hewani kwa ridhaa yako shughuri yako kwenye Mtandao huu unaotazwama na watu wengi pande zote za dunia. 
 
Mtandao huu unamuomba Mwenyezi Mungu aisimanie ndoa hiyo awaepushe na mabaya yote, wavumiliae madhaifu yao kwa maana ya kubebeana misalama, wakilisimamia kiapo chao cha ndoa cha kupendana mpaka kifo kitakapo watenganisha.

No comments:

Post a Comment

JUMBE WA LEO.

          “Ukichoka kutembea na Dunia. Dunia haitasimama kukusubiri.”   Pichani   Dunstan Shekidele akitembe na Dunia Wilaya   mbali...