Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Wednesday, July 7, 2021

BAADA YA KUKUTANA NA BABA MCHUNGAJI HARUSINI NAWIWA KUTOA USHUHUDA HUU.


 
Mchungaji Heliamini na mkewe wakiwa meza kuu upande wa wazazi wa Bwanaharusi ndani ya Ukumbi wa Mango Gardeni Morogoro hii ni mara baada ya kusalimiana na Mpiga Picha wa Mtandao huu.

 

Na Mwandishi Wetu, Morogoro.

KAMA ambavyo nilitangulia kudokeza kwenye stori iliyopita nikiwa harusini jana nilibahatika kukutana na baba Mchungaji Kachua Heliamani niliyepotezana naye kwa zaidi ya miaka 10.

Binafsi sikushangaa sana kupotezana kwa muda huo mrefu na mtumishi huyo wa Mungu anayeongoza waumini wa kanisa la Sabato lililopo Misufini Kata ya Mafiga.
Mosi Mkoa wetu wa Morogoro kwa sasa unakua kwa kiwango cha Mwendo Kasi.

Pili Mapito yetu ni tofauti, Kidhehebu yeye ni Msabato anayeabudu Jumamosi, na Mimi na MKKKT ninaye abudu Jumapili.

Tatu mara nyingi mimi natumia usafiri wa ‘bango’ boda boda’ yeye anatumia usafiri wa gari akitembea huku yuko ndani.

Nne kikazi Mimi nashinda Vijiweni na kumbi za starehe kusaka matukio, yeye kikazi anashinda Kanisani na kwenye mikutano ya dini kuwahubiria watu neno la Mungu.

Naludia tena kusema kutoka ndani ya sakafu ya Moyo wangu kwamba kwa kipindi chote cha miaka zaidi ya 10 toka Mkasa huu utokee sikipenda kusimulia Popote zaidi ya kubaki na machungu moyo.
Chaajabu jana nikiwa kwenye harusi ukumbi wa Mango Garden nafanya kibarua cha Kupiga Picha ili nipate mkate wa kujikimu kimaisha nilimuona Mchungaja Heliamini ambaye licha ya wote kuishi Manispaa ya Morogoro lakini hatujawahi kuonana zaidi ya miaka 10.

Hivyo macho yetu yalipogongana kila mmoja aliibua mshangao wa furaha huku tukasalimiana kwa kukumbatiana kila mmoja akimshangaa mwenzie na kumuliza kama anaishi Morogoro au la.

Yote jibu lilikuwa Moja tu nalo ni “bado naishi Morogoro mbona hatuonani sasa”.swali jilo hakuna aliyetoa jibu

Kwenye kisa hiki Mchungaji huyu anahusika kwa kuniuzia gari Mpya Mwaka 2007 na gari hilo baadae liliniletea matatizo Makubwa na mpaka naandika makala hii Mchungaji huyo hajuia kilichonikuta na mimi sikupenda kumueleza na kamwe sitamueleza nahisi nikimueleza ataumia sana.

Siku zote katika maisha yangu naongozwa na roho Mtakatifu, japo kwa miaka yote 10 sikupenda kuelezea mkasa huo ulionikuta,

chaajabu baada ya kumuona mchungaji huyo jana nikakumbuka matatizo liyonikuta na moja kwa moja ni kasukumwa na roho Mtakatifu kuandika Makata hii kudadavua kila kitu.

Nini kimetokea Makala hii itaendelea Kesho hivyo kamwe usiwe mbali na Mtandao huu

No comments:

Post a Comment

JUMBE WA LEO.

          “Ukichoka kutembea na Dunia. Dunia haitasimama kukusubiri.”   Pichani   Dunstan Shekidele akitembe na Dunia Wilaya   mbali...