Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Sunday, July 25, 2021

BAADA YA IHEFU KUSHUKA DARAJA TEPSI KUREJEA AZAM.

MCHEZAJI wa Azam Tepsi Evance anayeicheze lhefu kwa Mkoapo
Tepsi ''fundi' wa Mpira akimiliki Mpira mbele ya beki wa Salange juzi kwenye michuano ya The Gunners Ndondo Cup inayoendelea  uwanja wa Saba saba Morogoro


 

Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

BAADA ya timu ya lhefu yenye Maskani yake katikati ya Mashamba ya Mpunga  Mbalali Mkoa Mbeya kushuka daraja kutaka ligi kuu hadi ligi daraja la Kwanza.

 

Winga hatari wa timu hiyo Tepsi Evance aliyeitumikia timu hiyo kwa Mkopo akitokea Azam, amesema baada ya timu hiyo kushuka daraja aikacha timu hiyo na kurejea Azam.

 

Tepsi  Mkazi wa Kilakala Mkoani hapa aliyasema hayo juzi kwenye uwanja wa Saba saba aliposhiriki michuano bora ya The Gunners Ndondo Cup, akiitumukia timu ya Moro Kids iliyokipiga na Salange Fc kwenye mchezo wa Robo fainali.

 “Baada ya lhefu kupanda Ligi kuu Msimu uliopita mabosi  wangu wa Azam walinipeleka kwa mkopo hivyo kwa vile imeshuka daraja nitarejea nyumbani Azam”alisema Winga huyo.

 

lfahamike kwamba Tepsi akiwa na umri wa miaka 10 alikuwa Academy ya Mwere’ Maarufu Mwere Kids ya Mkoani Morogoro’ inayoongozwa na Ticha Tike Tike.

 

 Kwenye michuano ya Vijana chini ya Miaka 17 ya Coca Cola iliyofanyika jijini Dar huku Tepsi akiitumikia timu ya Mkoa wa Morogoro baada ya michuano hiyo kukamilika,Azam walivutiwa na kiwango cha mchezaji huyo  wakaamua kumvuta kwenye timu yao kikosi cha Pili na baadae walimtoa  kwa Mkopo kwenda lhefu.

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...