Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Monday, October 27, 2025

ABOOD APA KUPAMBANA NA WANAOCHAKACHUA PESA ZA WAJASILIAMALI.

                         Baadhi ya umati wawajasiliamali
Dkt Aziz Abood akizungumza na wajasiliamali wa Jimbo la Morogoro





                        Leones  Mvungu akifunga mkutano huo

 


           Na Dustan shekidele Morogoro.

MBUNGE wa Jimbo la Morogoro  MjIni kwa Leseni ya Chama cha Mapinduzi [CCM] Mhe Abdulaziz Mohamed Abood Almaarufu Aziz Abood,ameapa kupambana na baadhi ya watumishi wa serikali wanaotumia vibaya pesa za mikopo ya vikundi vya wajasiliamali zinazotolewa na serikali kuu ndani ya Jimbo lake.

 

 Mhe Abood  ametoa kauli hiyo ljumaa iliyopita ndani ya ukumbi wa Tanzanite uliopo eneo la Msamvu Mataa.alipokutana na Vikundi vya Wajasiliamali kutoka kata zote 29 za Jimbo la Morogoro Mjini.

 

“ Kabla ya kukutana na nyinyi hii leo nimefuatilia na kubaini kwamba pesa za mikopo kwa vikundi vya wajasiliamali nyingi haziwafikii walenga.

Pale ofisni utakuta mtumishi wa serikali anatengeneza kundi cha familia yake wanajikopesa hizo pesa” amesema mhe Abood na kukatishwa na shwange kubwa akishangiliwa na wajasiliamalia hao ambao wengi wao ni wanawake.

Baada ya shangwe hizo zilizodumu kwa takribani dakika 1 kunyamaza Mhe Dkt.Abood aliyeonyesha wazi wazi kukerwa na jambo hilo aliendelea kufunguka.

 

“ Nahidi tarehe 29 mkinichangua tena kwa kushirikiana na viongozi wangu wa chama yuko hapa katibu Mkuu nitashirikiana nao kupambana na watumishi hao na kuhakikisha wahusika ambao ndio nyinyi  mnapata mikopo hiyo tena kwa wakati kwa sababu hilo lipo ndani ya ilani ya chama ” alimalizia kusema Mbunge huyo na kupokea zawadi ya lundo la Vigeregere na makofi ya kutosha.

 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Vikundi  vya wajasiliamali hao Bw Leonis Mvungu akifunga mkutano huo alisema.

 

”Mhe Mbunge sisi wajasiliamali tunakupenda sana tazama juzi tu yaani siku mbili zilizopita ndio uliomba kukutana na hawa wajasiliamali kwa siku hizo chache umekuja umati huu mkubwa wengine wamejaa huko nje baada ya kukosa nafasi.

 

Naamini ungetuambia mapema wangekuja zaidi ya hawa”alisema Mvungu.

 

Akizungumza na Mtandao huu baada ya kutamatika kwa mkutano huo Mvungu alisema

”Mimi ninavikundi 390 na kila kukundi kina watu zaidi ya 20 shekidele wewe ni shahidi  hupo kwenye moja ya vikundi vyangu sina ubabaishaji kwenye shughuri hii”alisema Mvungu.

 

Mkutano huu umehudhuriwa na Katibu Mkuu wa CCM Mkoa wa Morogoro Bw Nuru John Ngereja.Katibu wa CCM Wilaya ya Morogoro Mjini Bw Twalib Berege na Katibu Hamasa,Uenezi na Uwezeshaji Bw Maulid Chambilila.

 

Mhe Abood ambaye pia ni Mfanyabiashara Maarufu Tanzania akimiliki Mabasi,Malori, Viwanda, Vyombo vya habari na Vituo vya Mafuta[Sheli] amechaguliwa kwa kishindo kwenye kura za maoni ndani ya chama chake cha CCM.

 

Kufuatia kuridhishwa na utendaji kazi wa Mbunge huyo wanachama wa CCM Jimbo la Morogoro Mjini kwa kauri moja wamempitisha kugombea tena kwa mara ya 4 mfurulizo, Mhe Abood aliingia Mjengoni Dodoma kwa mara ya kwanza 2010.

 

 

 

 

 

 

ABOOD APA KUPAMBANA NA WANAOCHAKACHUA  PESA ZA WAJASILIAMALI.

           Na Dustan shekidele Morogoro.

MBUNGE wa Jimbo la Morogoro  MjIni kwa Leseni ya Chama cha Mapinduzi [CCM] Mhe Abdulaziz Mohamed Abood Almaarufu Aziz Abood,ameapa kupambana na baadhi ya watumishi wa serikali wanaotumia vibaya pesa za mikopo ya vikundi vya wajasiliamali zinazotolewa na serikali kuu ndani ya Jimbo lake.

 

 Mhe Abood  ametoa kauli hiyo ljumaa iliyopita ndani ya ukumbi wa Tanzanite uliopo eneo la Msamvu Mataa.alipokutana na Vikundi vya Wajasiliamali kutoka kata zote 29 za Jimbo la Morogoro Mjini.

 

“ Kabla ya kukutana na nyinyi hii leo nimefuatilia na kubaini kwamba pesa za mikopo kwa vikundi vya wajasiliamali nyingi haziwafikii walenga.

Pale ofisni utakuta mtumishi wa serikali anatengeneza kundi cha familia yake wanajikopesa hizo pesa” amesema mhe Abood na kukatishwa na shwange kubwa akishangiliwa na wajasiliamalia hao ambao wengi wao ni wanawake.

Baada ya shangwe hizo zilizodumu kwa takribani dakika 1 kunyamaza Mhe Dkt.Abood aliyeonyesha wazi wazi kukerwa na jambo hilo aliendelea kufunguka.

 

“ Nahidi tarehe 29 mkinichangua tena kwa kushirikiana na viongozi wangu wa chama yuko hapa katibu Mkuu nitashirikiana nao kupambana na watumishi hao na kuhakikisha wahusika ambao ndio nyinyi  mnapata mikopo hiyo tena kwa wakati kwa sababu hilo lipo ndani ya ilani ya chama ” alimalizia kusema Mbunge huyo na kupokea zawadi ya lundo la Vigeregere na makofi ya kutosha.

 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Vikundi  vya wajasiliamali hao Bw Leonis Mvungu akifunga mkutano huo alisema.

 

”Mhe Mbunge sisi wajasiliamali tunakupenda sana tazama juzi tu yaani siku mbili zilizopita ndio uliomba kukutana na hawa wajasiliamali kwa siku hizo chache umekuja umati huu mkubwa wengine wamejaa huko nje baada ya kukosa nafasi.

 

Naamini ungetuambia mapema wangekuja zaidi ya hawa”alisema Mvungu.

 

Akizungumza na Mtandao huu baada ya kutamatika kwa mkutano huo Mvungu alisema

”Mimi ninavikundi 390 na kila kukundi kina watu zaidi ya 20 shekidele wewe ni shahidi  hupo kwenye moja ya vikundi vyangu sina ubabaishaji kwenye shughuri hii”alisema Mvungu.

 

Mkutano huu umehudhuriwa na Katibu Mkuu wa CCM Mkoa wa Morogoro Bw Nuru John Ngereja.Katibu wa CCM Wilaya ya Morogoro Mjini Bw Twalib Berege na Katibu Hamasa,Uenezi na Uwezeshaji Bw Maulid Chambilila.

 

Mhe Abood ambaye pia ni Mfanyabiashara Maarufu Tanzania akimiliki Mabasi,Malori, Viwanda, Vyombo vya habari na Vituo vya Mafuta[Sheli] amechaguliwa kwa kishindo kwenye kura za maoni ndani ya chama chake cha CCM.

 

Kufuatia kuridhishwa na utendaji kazi wa Mbunge huyo wanachama wa CCM Jimbo la Morogoro Mjini kwa kauri moja wamempitisha kugombea tena kwa mara ya 4 mfurulizo, Mhe Abood aliingia Mjengoni Dodoma kwa mara ya kwanza 2010.

 

 

 

 

 

 

Tuesday, October 21, 2025

KIJIWE NONGWA. UKIONA KAFUTA BANGO UJUMBE UMEFIKA



















Na Mpekunyuzi wa Mitandaoni Dunstan Shekidele.

Kama kawaida mtumishi wako, kila wiki naweka Bando linalonitembeza kwenye Mitandao ya Kijamii kukusanya jumbe mbali mbali.

Miongoni mwa jumbe hizo ni za Kuelimisha, Kukosoa na Maneno ya hekima yanayotukumbusha kutenda mambo  mema.

Kwa jumbe nyingine mbali mbali tukutane wiki ijayo panapo majaliwa ya Mwenyezi Mungu



KIJIWE NONGWA. UKIONA KAFUTA BANGO UJUMBE UMEFIKA

Na Mpekunyuzi wa Mitandaoni Dunstan Shekidele.

Kama kawaida mtumishi wako, kila wiki naweka Bando linalonitembeza kwenye Mitandao ya Kijamii kukusanya jumbe mbali mbali.

Miongoni mwa jumbe hizo ni za Kuelimisha, Kukosoa na Maneno ya hekima yanayotukumbusha kutenda mambo  mema.

Kwa jumbe nyingine mbali mbali tukutane wiki ijayo panapo majaliwa ya Mwenyezi Mungu



Tuesday, October 14, 2025

NYERERE DAY.



LEO Octobar 14.2025 Mwasisi Mzalendo wa Taifa la Tanzania Mwalimu Juliusi Kambarage Nyerere'Baba wa Taifa'.ametimiza miaka 26 toka alipofariki dunia Octobar 14 1999.
Mwandishi wa habari hizi anamuenzi baba wa Taifa kwa kuendesha Baiskeri.


 

Friday, October 10, 2025

BABU KICHUYA AKAGUA UJENZI WA DARAJA,

           Muonekano wa daraja la zamani baada ya kukatika
             Babu kichuya akikagua daraja hilo jana mchana



Jengo  linaloonekana kwa  mbali lenye paa la vigae vyekundu ni eneo a Stesheni ya Morogoro
Babu Kichuya kushoto akiwa na Mwandishi wa habari hizi wakijiandaa kuelekea darajani

                             .......Safari ya kuelekea darajani akianza


              Na Dustan Shekidele,Morogoro,  

Mzee Ibrahim Mohamed  Mangwende Almaarufu ‘Babu Kichuya’  amekagua ujenzi wa daraja la Relwe Maarufu daraja la Ng’ombe lililopo mtaa wa Makaburi ‘A’ Kata ya Mji Mpya Mkoania hapa.

 

Jana majira ya mchana Mzee huyo akiwa na Mwandishi wa habari hizi wakitumia usafiri wao wa baiskeri walitinga kwenye daraja hilo na kushuhudia Mkandarasi akiwa Site akiendelea na kazi kwa kasi ya kuridhisha.

 

Akizungumza na Mtandao huu mara baada ya kukagua daraja hilo ambalo lipo mto Morogoro mzee huyo alisema.

 

” Mimi ni mwananchi wa Morogoro niiyekulia Mji Mpya nimeamua kuja kukagua ujenzi wa daraja letu ama kwa hakika nimefurahishwa na kazi nzuri inayondelea kwenye mradi huu,kipekee naipongeza serikali yetu kwa ujenzi wa daraja hili litakalofungua barabara hii muhimu ya kuelekea kichangani”alisema babu kichuya ambaye ni fundi bomba mstaafu wa Mamlaka ya Maji safi na Maji taka Mkoa wa Morogoro’MORUWASA’

 

Ifahamike Mzee huyo mmoja wa wamjuu zake ni mchezaji nyota wa Maafande wa JKT Tanzania Shiza Ramadhan Kichuya aliyewahi kutamba na Simba kabla ya kutimkia Misri kucheza Soka la Kulipwa.

 

    KWA NINI LIITWE DARAJA LA NG’OMBE?

Miaka ya nyumba wakati Mwandishi wa habari hizi anasoma shule ya Msingi Kaloleni iliyopo  jirani kabisa na daraja hilo,walishuhudia Makundi ya Ng’ombe yakivushwa kwenye daraja hilo dogo linaloonekana pichani yakitokea Machinjio ya Morogoro yaliyopo Mtawara wakipelekwa Stesheni ya Morogoro inayoonekana kwa mbali yenye vigae vyekundu.

 

Baada ya kufika stesheni hapo Ng’ombe hao hupakiwa kwenye Treni ya Mizigo na kupelekwa Machinjio ya Ng’ombe  Vingunguti Jijini Dar es salaam.  

 

Takribani miezi 5 iliyopita daraja hilo lilikatika na kukata mawasiliano ya pande mbili, huku Mtandao huu ukiwa wa kwanza kuripoti habari hiyo.

 

Baadae Mkandarasi wa daraja hilo alijenga daraja a muda linaloonekana pichani sambamba na Mkandarasi huyo kuanza kwa  kwa kasi  ujezi wa daraja kubwa huku akiwa kwenye hatua za mwisho za kulikamilisha kama.

 

 

 

 

 

VITUKO VYA MWEZI JANUARI

  Mwezi uliopita tumeshehelekea Siku Kuu mbili X Mas na Mwaka Mpya.   Mwezi huu dume January tunashehelekea kulipa Ada za Shule na kod...