Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Friday, July 11, 2025

KAZI INAENDELE KWA KASI MKANDARASI KAMUA KULING’O LILE DARAJA LILILOKATIKA,

              Daraja  la zamani baada ya kukatika hali ilikuwa hivi
Madent wa Shule ya Msingi Kaloleleni wakigombea kuvuka kwenye daraja hilo la muda



           Muonekana wa sasa baada ya daraja la awari kuondewa

         

           Na Dustan Shekidele.Mogoro

ILI kupata uwanja mpana wa kufanya kasi kwa haraka, wakandarasi wa Kampuni ya COPE iliyopewa jukumu la kujenga daraja kubwa a Relwe Maarufu daraja la Ng’ombe ameamua kuliondoa daraja la zamani na kutengeneza daraja la muda upande wa kulia wa Mto Morogoro.

 

Ikumbukwe mwezi ulipita daraja hilo lilikatika na kukata mawasiliano ya watumiaji wa daraja hilo wananchi wa kata za Mji Mpya na o Kichangani.

 

Hali hiyo ilisababisha usumbufu kwa watu mball ikiwemo wanafunzi wa shule za Sekondari na Msingi pamoja na wazee wasiojiweza wanaotunzwa na serikali kwenye  kambi ya Funga funga.

 

Juzi Mtandao huu  ulitinga kwenye daraja hilo kwa lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa daraja hilo na kuwahabarisha wananchi  hususani wananchi wa kata za Mji Mpya na Kichangani wanautumia daraja hilo ambalo ni kiunganishi muhimu cha kata hizo mbili ambazo ni Maarufu Mkoani  Morogoro.

 

Baada ya kufika Mtaa wa Makaburi ‘A’ kata ya Mji Mpya lilipo daraja hilo Mtandao huu ulishuhudia watu mbali mbali wakiwemo wanafunzi wa shule ya Msingi Kaloleni wakigombea kuvuka kwenye daraja  la Muda kama wanavyoonekana pichani.

Wahenga wanasema ‘kujisifu sio dhambi  dhambi ni kuziendekeza hizo sifa’.

 

Mara baada ya daraja hilo kukatika Mtandao ndio ulikuwa wa kwanza kuripotia habari hiyo.sasa hapa siziendekezi hizo sifa ndio maana naendele kuwapa mwendelezo wa ujenzzi wa daraja hilo mara kwa Mara.

 

Mtandao huu utafanya hivyo mpaka daraja hilo litakapokamiika.

 

No comments:

Post a Comment

MAKALA PLANET NDONDO CUP. SIRI DAMU CHAFU KUTWAA UBINGWA MARA MBILI MFURULIZO HII HAPA.

  Baadhi ya mashabiki waliofulika kwenye mashishindano hayo.                           .....Kikosi cha Damu chafu Mkuu wa Wilaya Mhe Kilakal...