Mkuu wa Wilaya Mhe Mussa Kilakala akizungumza kabla ya gemu hiyo kuanza
Warembo wakiingiza kombe uwanjani
kiksosi cha Damu Chafu kiichoanza juzi Shiza Kichuya alingia kipindi cha pii
Rais wa Damu Chafu Ayub kati dakika zote 90 alikuwa bize na vijana wake kuzunguka uwanja wa saba saba. Alipofika gori la kaskazini mwa uwanja alisimama na kusalimiana na Mpiga picha wa Mtandao huu
Sales Manager wa Kings Super Brands Limited Geofrey Karumura kulia akimkabidhi Mfano wa hundi ya Milion Mbili Nahodha wa Chaka Bovu Fc George Chota
.....Mhe Mussa Kilakala kushoto akimkabidhi mfano wa hundi ya Milion 4 Nahodha wa Damu Chafu Sady Mapuya
,,,,Nahodha wa Makombe Sady Mapuya akiwa na kombe
Mabingwa Damu Chafu wakiwa na Mwali wao
Na Dustan Shekidele Morogoro.
TIMU ya Damu Chafu Fc ikiongozwa na Shiza Ramadhan Kichuya’ Mzee wa Kona gori’ jana wamefanikiwa kutetea ubingwa wa Michuano ya Planet Ndondo Cup 2025,baada ya kuinyuka timu ya Chaka Bovu Fc ‘Vijana wa Nickson Kibabage kwa bao 3-0.
Hadi dakika 45 za awari zinatamatika kwenye gemu hiyo iliyopigwa uwanja wa Saba saba na kushuhudiwa na Umati Mkubwa wa mashabiki walioongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe Mussa Kilakala washindi walikuwa mbele kwa bao 1-0 zilizopachikwa dakika ya 12 na Clement Mshasha mchezaji wa zamani wa Singida Big Stars.
Chama la Masela Damu Chafu ambao mwaka jana wakiwa na beki wa Simba Abdrazack Spear Hamza walitwa ubingwa huo kwenye uwanja huo huo wa Saba saba walikianza kipindi cha pili kwa kasi ya SGR na kufanikiwa kuongeza mabao mawili ya haraka haraka.
Baada ya gemu hiyo kutamatika Mgeni Rasmi Mhe Mussa Kilakala alimkabidhi kombe Nahodha wa Damu Chafu Sady Mapuya na kiticha cha pesa Milioni 4 kwa mfumo wa hundi.
Nahodha wa Chaka Bovu George Chota anayeitumikia Mtibwa Sugar alikabidhiwa Milioni 2 na Geofrey Karumuna ambaye ni Meneja Mauzo wa kamuni ya Kings Super Brands Limited.
Kampuni hiyo inayojihusisha na utengenezaji wa Pombe ni mmoja ya wadhamini wa mashindano hayo yaliyoshirikisha timu 4 za Black People, Damu Chafu, Wakushi na Chaka Bovu.
Wakihojiwa na Planent Redio siku mbili kabla ya fainali hiyo Viongozi wa Chaka Bovu walisema kwamba endapo wangefanikiwa kutwaa ubingwa huo na kukabidhiwa kitita hicho cha Milioni 4 wangefanya yafuatayo,
Mosi wangetoa sadaka ya kununua Luku ya elfu 50 kwa misikiti 5 kila msikiti mmoja ikipewa Luku ya elfu 50,
Pili wangeso duwa ya kuwarehemu marehemu ambapo dua hiyo ingekwenda sambamba ba sadaka ya chakula’
Chaka Bovu walitinga fainali baada ya kuwafunga Wakushi na Damu chafu waliwafunga Black People.
Wiki iliyopita Mtandao huu ulikutana na Rais wa Black People Seif Kijiji nyuma ya Kanisa la TAG Mwembesongo na kumuliza sababu za kufungwa na Damu Chafu alijibu hivi.
“Shekidele kwenye gemu ile nilicheza na timu nne kwa mpigo ndio maana nimezidiwa Damu Chafu alisaidiwa na timu za Chadongo, Burkinafaso na Asseple Fc timu zote hizo zinatoka Mafisa kata ya Mwembesongo n azote zimekufa ila viongozi wao wapo” alisema Seif.
Kama kawaida Mtandao huu umekusanya matuki kibao kwenye fainai hiyo hivyo endelea kuwa jirani na mtandao huu muda wote.
No comments:
Post a Comment