Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Monday, May 26, 2025

YAMETIMIA,KAZI INAENDELEA.




 


 Na Dustana Shekidele, Morogoro.

HATIMAYE Ujenzi wa daraja kubwa mto Morogoro eneo la Maghorofa ya Reli makutano ya Kata kubwa za Mji Mpya na Kichangani umeanza juzi.

 

Ikumbukwe siku za hivi karibuni Mtandao huu uliripo kwa undani ujenzi wa daraja hilo linalotajwa kuwa Mwarobani wa foleni za vyombo vya moto katikati ya Mji wa Morogoro.

 

Kwamba daraja hilo litakapokamilika watu watakao tokea barabarani ya Korogwe inayotoka Stend ya Msamvu kuelekea Kichangani, Kilakala.Kigurunyembe. Bigwa. ‘Kambi ya kulelea Wazee wasio jiweza ‘Funga Funga’.Gereza la Manispaa,  FFU Mkoa wa Morogoro’kikosi cha kutuliza ghasia cha Jeshi la Polisi’hawata lazimika kuingia katikati ya Mji badala yake watatumia daraja hilo wakiingilia Simba Oil kanisa la KKKT Usharika wa Mji Mpya wakivuka stend ya daladala ya Kaloleni Mji Mpya.

 

Jana Mwandishi wa Mtandao huu alishuhudia wanafunzi wa shule ya Msingi Kaloleni wakishuhudia Mtambo’Kijiko’ cha Mkandarasi kikiendelea na kazi ya ujenzi wa daraja hilo.

 

  Juhuzi za Mwandishi wa habari hizi za kutaka kuzungumza na Mkandarasi wa daraja hilo ziligonga Mwamba kwa sababu hakuwe eneo la tukio juhuzi hizo za kumsaka zinaendelea.

 Habari za awari zilizopatikana eneo la tukio  zinadai Mkandarasi huyo atakamilisha ujenzi wa daraja hilo ndani ya miezi minane’8’.

 Awari eneo hilo lilikuwa na daraja dogo lenye uwezo wa kupitisha, Pikipiki, Baiskeli na watembea kwa Miguu.  

Daraja hilo litakapokamilika kitachongwa kipande cha barabara kutoka barabara ya Lami ya Kichangani ikikatiza kando kando ya Uwanja wa Mazoezi wa timu ya Reli ya Morogoro, jirani na Shule ya Msingi Kaloleni ikifika kwenye daraja hilo inaungana na barabara ya kuelekea KKKT.

 

Kwa sasa kipande hicho cha upande wa pili wa kichangani hakina barabara, iliyopo ni ya watembea kwa miguu, Baiskeli na pikipiki.

No comments:

Post a Comment

MAKALA PLANET NDONDO CUP. SIRI DAMU CHAFU KUTWAA UBINGWA MARA MBILI MFURULIZO HII HAPA.

  Baadhi ya mashabiki waliofulika kwenye mashishindano hayo.                           .....Kikosi cha Damu chafu Mkuu wa Wilaya Mhe Kilakal...