Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Monday, April 22, 2024

KUMBUKIZI YA MIAKA 11 YA KIFO CHA MKALI WA HIP HOP ‘NGWEHA’

           Hayati Mangweha enzi za uhai wake.
Denisia Mangweha ambaye ni Mama Mzazi wa hayati Albert Mangweha akihojiwa na Mtandao huu nyumbani kwake Kihonda Mazimbu Road Morogoro huku akiikumbatia picha ya Mpendwa Mtoto wake, huku akiwa na majonzi makubwa.
Paroko wa Parokia ya Mt. Monica Padre Octavian Msimbe[kati] akiwa na Micheli Raia ya Uingereza[kushoto] mchumba wa hayati Ngweha.

[Kulia] ni Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya Hamza Mgaza’ Maarufu M- 2- THE- P ambaye ni rafiki mkubwa wa hayati Mangweha, watatu hao walipozi mbele ya kamera za Mtandao huu kwenye lbada ya kumbukizi ya mwaka mmoja wa kifo cha hayati Mangweha Mei 28-2014



 Mwandishi wa habari hizi akiwa kwenye kaburi la Mangweha nje ya kanisa  Katoliki Parokia ya Mt Monica Kihonda.


           Na Dustan Shekidele,Morogoro.

 Kumbukizi ya Miaka 11 ya kifo cha Mkali wa muziki wa Bongofleva nchini,  Mwana Morogoro Hayati Albert        Keneth Mangweha’Ngwea’ aliyefariku dunia  Mei 28=2013  nchini Afrika Kusini, na kuzikwa nyumbani kwao Morogoro  kwenye makaburi yaliyopo nje ya kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro Parokia ya Mt Monica Kihonda.

Watanzania wengi haswaa Wana Morogoro watakukumbuka daima kamanda Ngwea umeipeperusha nyema bendera ya Mkoa wa Morogoro kwenye tasnia hiyo ya Muziki wa kizazi Kipya miondoko ya ‘Hip Hop’.  

Moja ya wimbo wako uliotia fora nchini ni ule wa ‘Geto langu’         

Panapo Majaliwa ya Mwenyezi Mungu Mei 28 2024 Mwandishi wa Mtandao huu atatinga nyumbani kwa Mama Mangweha ambaye ni mmoja wa viongozi wa Parokia ya Mt. Monica, kushiriki lbada ya kumbuki ya miaka 11 ya kifo cha Mangweha.

Baada ya lbada hiyo nitazungumza  mawili matatu na Mama Mangweha kuelekea miaka 11 ya kifo cha mpendwa mtoto wake huyo aliyekuwa kipenzi cha Watanzania wengi.

Hivyo nakusihi endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote.  

                        

  .

 .

 

 

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...