Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Sunday, February 5, 2023

KUMBUKIZI MWANAMUZIKI AFUNGUKA KUIMBA NJIMBO ZA INJIRI NA BONGOFLEVA.



 MASTAA wa nyimbo za lnjiri nchini kutoka kulia ni Bahati Bukuku[kati[ Matha Mwaipaja na kushoto ni Stara Thomas,Wakipozi mbele ya Camera za Mtandao Pendwa wa Shekidele.


 

Mwandishi wa Mtandao huu kulia akimuweka Mtu kati Msanii nyota wa lnjiri[Muziki wa kumtukuza Mungu’ na Muziki wa kizazi Kipya’Bongofleva’ Stara Thomas.

Kwenye mahojiano hayo aliulizwa swali, kwa nini anakuwa vuguvugu Moto si Moto baridi si baridi kwa maana mchana anaimba nyimbo za kumtukuza Mungu na Usiku anaimba nyimbo za Bongofleva nyimbo za kidunia,kwamba kiimani jambo hilo limekaaje kwa upande wake?

Swali hilo lilionekana kumzidi kimo ambapo alipotakiwia kujibu muda mwingi aliutumia kuchezea macho yake na mwisho akajibu kwa kifupi akisema.

” Swala hilo limekaa vibaya so muda wowote kuanzia sasa nitaachana na muziki wa kidunia na kubaki kwenye kazi Moja ya kumtumikia Mungu wangu ambaye ni Mwaminifu kwangu”

 

 

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...