Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Wednesday, November 9, 2022

KUMBUKIZI MSIMU WA EMBDE DODO HUYOOOO



 

 .

Msimu wa embe dodo unakaribia hili sio dodo la  Msanii Ally Kiba ule wimbo wake wa dodo hapana.

Miaka ya hivi karibuni nilifanya ziara ya  kutembelea Tarafa ya Matombo Kijiji cha Mkuyuni Wilaya ya Morogoro Vijijini msimu wa embe nikakutana na mkulia akiuza  dodo moja shilingi mia 2.

 

Mkulima huyo aliyepanga embe zake kando kando ya barabara kuu ya kutoka Morogoro Mjini eneo la Bingwa kuelekea Kisaki alisema mteja akinunua embe zaidi ya kumia bei inapungua atauza moja shilingi 100.

 

Mpiga Picha wa Mtandao huu alitoa buku 2 akakusanyiwa dodo Mdonde zilizoivia mtini 20 akafunga kwenye Piki piki  yake na kurejea nazo Mjini Morogoro.

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...