Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Tuesday, August 30, 2022

UTANI WA JADI,KWENYE DRAFT KIJANA AMPA ADHABU YA KUBEBA JIWE MZEE WAKE.



 


             Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

Kijana mmoja Mfanyabiashara Maarufu wa Mitumba Mkoani Morogoro Jose Matei’Maarufu ‘Juto Mitumba’amempa adhabu ya kubeba jiwe, Salum Said Maarufu Mzee Kipese’baada ya kumfunga bao 6-0 kwenye mchezo wa Draft.

 

Tukio hilo lililojaza watu wengi limetokea hivi karibuni kwenye Soko la Nguo Maarufu Mnada wa Saba saba uliopo Kata ya Saba saba Manispaa ya Morogoro,ambapo wawili hao walikubaliana kwele ya ushahidi wawatu kwamba wacheze Draft  sharti la  atakayenza kufungwa bao 1 atapewa adhabu ya kubeba jiwe huku anacheza mchezo huo kwa mkono mmoja mpaka atakapo komboa bao hilo.

 

Hivyo walipoanza Mzee Kipesa alifungwa bao moja na Juto  katafuta jiwe kubwa na kumbebasha Mzee huyo bila huruma, Mzee kipese alijipapatua kurejesha bao hilo  bila mafanikio na kujikuta akiongezwa mabao mengine 5,uzito ulivyozidi dingi huyo alitupa jiwe hilo na kuondoka zake huku Vijana wakimsindikiza na maneno ya utani.

 

 Mzee Kipese aliwajibu kwamba anakwenda kula ugari kwa mkewe akirejea atakuwa na nguvu na akili Mpya.

 

”Huyu Majuto hana uwezo  kanifunga kwa sababu ya uchovu na Njaa bibi yeni kanitumia meseji ugari ukotayari ngoja nikale nikirudi nitalipa kisasi cha kumbebesha jiwe Majuto”alisema Mzee Kipese huku akiondoka zake.

 

Alipohojiwa na Mtandao huu Mzee Kipese alikiri kufungwa kasha kibabeshwa jiwe na Majuto.

 

Kwa upande wake Majuto anayemiliki banda la Mitunda katikati ya Mji wa Morogoro jirani na Ofisi kuu za kampuni ya Mabasi ya Abood alisema uwezo wake kwenye mchezo huo ni wakiwango cha juu.

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...