Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Saturday, July 16, 2022

BODA BODA HAIACHI KITU INASAFIRISHA KILA KITU IKIWEMO MAITI NA KITI MOTO.






 


 

 

                  Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

 

 

 USAFIRI  wa boda boda  umekuwa mkombozi Kwa watu wengi wa kipata cha chini hasa wale waishio Vijijini.

 

 Mwandishi wa mtandao huu ambaye naye hutumia usafiri huo wa Booda boda kwenda Wilayani mbali mbali za Mkoa wa Morogoro kwa lengo la kuripoti habari zinazowahusi watu wanyonge waishio  Vijijini.  

Mwanahabari huyo aliyejitoa mhanga kuwasaidi wananchi hao wa Vijiji kupaza sauti zao kwenye changamoto zinazowakabili.

 

Akiwa huko Vjijini Mwanahabari huyo amekutana na matukio mengine ya adha za usafiri na ubovu wa barabara.

 

 Uchunguzi wa Mwandishi wa habari hizi kwenye safari zake za huko vijijini umebaini Usafiri wa Pikipiki Maarufu boda boda umekuwa msaada mkubwa kwa wananchi wengi waishia maeneo hayo.

 

Mwandishi huyo wa habari za kijamii na kiuchunguzi alibaini usafiri  wa boda bado hutumika kama gari la wagonjwa [Boda boda Ambulance Village] kusafirisha maiti kutoka kijiji kimoja kwenda kijiji kingine, pia huwakimbiza  Wagonjwa wakiwemo wajawazito nyakati zote kwa maana Usiku na mchana kuwakimbiza vituo vya Afya.

 

Vile vile boda boda hizo hutumika kusafirisha Wanyama, Mazao hasa vyakati za mavuno pamoja na bidhaa za Madukani.

                       CAPTION

Picha no 1 Mwandishi wa Mtandao huu alimnana boda boda huyu akisafirisha maiti kutoka Moja ya Kijiji kilichopo Mpakati mwa Mikoa ya Tanga na Morogoro Kilindi Wilaya ya Kilongwe na Turiani Wilaya ya Movomero.

 

 Picha no 2 Mwandishi wa Mtandao huu alimna boda boda huyu akiwa na Lumbeza za bidhaa za dukani  akizisafiri kutoka Mnadani Kijiji ch Mlali Mgeta kuelekea dukani  kijiji cha Vitonga.

 

 

Picha no 3 Boda boda alinaswa akisafirisha Mnyama Nguruwe .a.k.,a Kiti Moto haijafahamika mara moja alipotoka na anapoelekea kwa kwa sababua baada ya kusimamishwa na Mwandishi wa habari hizi aligoma kusimama.

 

 Picha no 4 Mwandishi wa Mtandao huu akiwa moja ya Vijiji vya Mkoa wa Morogoro akitiza majukumu yake.

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...