Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Thursday, June 30, 2022

KIJIWE NONGWA. UKIONA KAFUTA BANGO UJUMBE UMEFIKA

















 


 

                          Na Mpekunyuzi wa Mitandao Dunstan Shekidele.

 

Kama kawaida mtumishi wako kila wiki naweka Bando linalonitembeza kwenye Mitandao ya Kijamii kukusanya jumbe mbali mbali.

 

 Miongoni mwa jumbe jizo ni  za  Kuelimisha, Kukosoa na Maneno ya hekima yanayotukumbusha  kuwa jirani na Mwenyezi MUNGU.

 

Tukutane Wiki Ijayo kwa mabango Mengine yenye Jumbe Moto Moto.

NYUMBA YA KADA WA CCM ILIYOKUWA NA MGONJWA NDANI IMETEKETEA KWA MOTO.

Mtandao huu unatoa shukrani za dhati kwa Maafande wa Kikosi cha Jeshi la Zima Moto baada ya kumpa ruhusa ya kupanda juu ya gari lao na kupiga Picha hiyo inayoonekana kwa uzuri zaidi
Mmiliki wa nyumba hiyo Kada wa CCM Nasma Ndehere akitoa maelezo kwa Afande wa kikosi cha Zima Moto
Afande wa kikosi cha Jeshi la Zima Moto na Uokoaji  Mkoa wa Morogoro akiendelea kuzima Moto kwenye moja ya vyumba vya nyumba hiyo





Ponge za kipee zimfikie Afande huyu aliyefika mapema eneo la tukio la kulinda mali zilizokuwa zikiokolewa kutoka kwenye nyumba hiyo.
....Afande huyo akimfariji Mmili wa nyumba hiyo Bi Nasma Ndehere
..Mmoja wa wapangaji aliyedaiwa kujiandaa kuhama kwenye nyumba hiyo akiangua kilio baada ya baadhi ya vitu vyake kuteketea kwa Moto.
Katibu Mwenyezi wa CCM Kata ya Mji Mpya Seleman Kasanga shati jekundu] akimsaidia mpangaji huyo kuokoa vitu kutoka kwenye janga hilo la  Moto
 

 


 

 

                                   Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

 

 INAUMA SANA.

Nyumba ya Nasma Hamisi Ndehere ambaye ni Kada Maarufu wa Chama Cha Mapinduzi’CCM’ Kata ya Mji Mpya Mkoani hapa, imeteketea kwa Moto huku mgonjwa aliyekuwa amelala ndani akinusurika baada ya kuokolewa na majirani.

 

 Tukio hilo la kuhudhunisha limetokea jana mchana kwenye nyumba hiyo ya familia ya Ndehere iliyopo Mtaa wa Makaburi B kata ya Mji Mpya.

 

 

Mwandishi wa Mtandao huu aliyekwenda kumsalimia Bi.mkubwa wake anayeishi   kwenye Mtaa huo. alishuhudia watu wakikimbia huku wakipiga kelele za nyumba inaunga.

 

Mwandishi wa habari hizi naye alikurupuka na kutinga eneo la tukio na kushuhudia moto huo ukianza kushika kasi, Moja kwa moja Mwandishi huyo alipiga simu Kikosi cha Zima Moto na Uokoaji kupitia namba yao ya bure’Emergency Number’ ya 114.

 

 Ndani ya dakika chache maafande hao wa  Zima Moto walitinga eneo la tukio na kuzima moto huo ambao tayari ulikuwa umeshateketeza vyumba 2.

 

 

Akizungumza na Mtandao huu kada huyo wa CCM  ambaye pia ni Mshereheshaji ’Mc’ Maarufu Mkoani Morogoro alisema.

 

”Nilikuwa kwenye shughuri zangu Mtaani nimepigiwa simu nikijulishwa  nyumba yetu inaungua moja kwa moja nilimuwaza mgonjwa wangu aliyekuwa amelala ndani na pesa za watu za mchezao Laki 2 zilizozihifadhi chumbani.

 

 

“Nashukuru nimefika hapa nimekuta majirani zangu wamemuokoa Mgonjwa na kwa vile moto ulikuwa haujafika chumbani kwangu nilimtuma kijana  kazitoa pesa hizo”alisema Mc Nasma ambaye pia ni Mke halali wa Hamis Ndehere.

 

Katika hatua nyingine Mc Ndehere alimuelekeza kwa hema Mpangaji wake aliyekuwa akifoka baada ya Moto huo kuunguza baadhi ya vitu vyake.

 

 

Mpangaji huyo Pichani anayeangua Kilio, kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana eneo la tukio alikuwa akijianda kuhama kwenye nyumba hiyo alikuwa akisubiri Muda  ufike kama utamaduni wetu ulivyo wa kuhama majira ya Usiku.

Kwa bahati mbaya wakati akisubiri hilo na yeye akiwa kwenye ,majukumu yake Mtaani alipigiwa simu akijulishwa tukio hilo la Moto.

 

 

Aliwasili eneo la tukio kwa usafiri wa boda boda na moja kwa moja alikimbilia chumbani wake kuokoa baadhi ya vitu  huku akiangua kilio akitaka kulipwa vitu vyake vilivyoungua.

 

 

Mama mwenye nyumba Mc Nasma baada ya kumsikia mpangaji wake huyo akifoka alimfuata  na kumueleza kwa hekima.

 

 

“Nimekusikia ukilia huku ukilalamika ukitaka kulipwa  vitu vyako,hakuna mtu aliyependa nyumba kungua hii ni ajari kama ajari nyingine hivyo unavyolalamika kungua kwa vitu vyako, wakati na mimi ninauchungu nyumba yangu kungua”.

 

 Maneno hayo ya hekima yalimgusa mpangaji huyo na Mwandishi wa Mtandao huu alimsikia mpangaji huyo akisema neno moja tu.

 

“ sawa mama lakini vitu hivi vichache nilivyookoa haviludi tena kwenye nyumbani hii naita gari naondoka zangu.”

Mwenye nyumba huyo hakumjibu chochote mpangaji wake huyo na badala yake aliondoka eneo hilo na kwenda kutoa maelezo  ya tukio hilo kwa maafisa wa Kikosi cha Zima Moto. Mtandao huu uliwashuhudia Vigogo kibao wa CCM Kata ya Mji Mpta wakishiriki kumsaidia Kiongozi mwenzao kwenye janga hilo.

 

Baadhi ya Kigogo hao wa CCM walioshuhudia na Mwandishi wa habari hizi ni pamoja na Mwenyekiti wa CCM kata ya Mji Mpya Said Kondo, Katibu Mwenezi Kata Seleman Kasanga, na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Simu C kata ya Mji Mpya kwa leseni ya CCM  Said Mkwinda ambaye pia ni Mwenyekiti wa tawi kuu la Simba Mkoani Morogoro.

 

.

Hadi tuna kwenda mitamboni chanzo cha Moto  huo hakijajulikana na hakuna mtu aliyefariki wala kujeruhiwa zaidi ya baadhi ya mali kuteketezwa na Moto huo. 

Wednesday, June 29, 2022

WAKATI LIGI KUU IKIFIKA TAMATI LEO. MORO KIDS WAIBUKA USAJIRI KIPA WA YANGA.



 


 

                               Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

 

 

 WAKATI msimu wa ligi kuu Tanzania Bara, ukifika tamati leo, Uongozi wa Taasisi Maarufu nchini ya kuibua na kukuza vipaji vya wachezaji ya Moro Kids  ya Mkoani hapa,wameibuka na kudai Pesa yao  ya Usajiri wa Kipa mpya wa Yanga Abuutwarib Msheri.

 

 

Majuzi Mwandishi wa Mtandao  huu akiwa kwenye mishe mishe zake za kusaka matukio alipigiwa simu na Mratibu Mkuu wa Taasisi hiyo Rajab Kindagule akimwalika kufika kwenye taasisi hiyo.

 

”Shekidele tunajua Mtandao wako unawasomaji wengi, njoo hapa Mazoezini kwetu Uwanja wa Shujaa tukupe habari inayomhusu Kipa wa Yanga Msheri”

 

 Fasta Mwandishi wa Mtandao huu alitinga eneo la tukio na Moja kwa moja Mratibu huyo alifunguka haya.

 

”Kama taasisi tumekuita kutoa lalamiko letu ligi kuu inafika tamati jumatano Mpaka leo Mtibwa hawajatulipa pesa yetu waliyomuuza Kipa Msheri kwenda Yanga kama tulivyokubaliana kwenye mikataba yetu”.alisema Kindagule na kuongeza.

 

 Haya tunayaona siku hizi lakini enzi la Uongozi wa Jamal tulikuwa tunalipwa haki yetu kwa wakati wanapomuuza mchezji wetu wanatupa haki yetu, nakumbuka mzozo ulianzia kwa Dickson Job tulihangaika sana kulipwa pesa yetu mpata tulivyowapeleka Mtibwa Takukuru ndio wametulipa Malipo ya Job.

 

 Kama taasisi tumeona lalamiko letu tulipeleke kwenu Waandishi wa habari mtusaidie kupaza sauti”amemalizia kusema Mratibu huyo ambaye ni Mwamuzi Mstaafu wa ligi Kuu Tanzania Bara.

 

Alipouliza Malipo hayo wanayoda ni kiasi gani, alisema makubaliyao yao kwenye mkatani wa Kipa huyo ni kwamba atakapouzwa popote Moro Kids watalipwa asilimia 25 ya pesa za mauzo.

 

 Alipoulizwa swali la pili kwa sasa taasisi hiyo ya Moro kids inawachezaji wangapi waliobaki kwenye kikosi hicho cha Mtibwa kwa sasa. alijibu

 

 “Tunawachezaji kama watano hivi kwenye kikosi cha Mtibwa na kwenye kikosi chao cha pili asilimia 80 ya wachezaji wote wa timu B ya Mtibwa wanatoka kwenye taasisi yetu.

 

Baada ya kusikia malalamiko hayo jana Mwandishi wa habari hizi aliwatafuta Viongozi wa Mtibwa kwa njia ya simu kwa lengo la kusikia kauli yao juu la lalamiko hilo zidi yao.

 

 Aliposomewa malalamiko hayo na kutakiwa kuyatolea majibu Kiongozi wa Mtibwa aliyejitambulisha kwa jina Moja la Abubakar alisema.

 

” Ni kweli Moro kids wanatudai hiyo pesa ila utaratibu walioutumia wa kuja kwenu Waandishi wa habari binafsi sikuupenda na juzi tu nimeongea na Kindagule nikimuomba waendelee kutuvumilia”alisema Kiongozi huyo.

 

 Alipoulizwa kwa nini wasilipe deni hilo ili hali wameshamuuza mchezaji huyo? Kiongozi huyo alijibu.

 

”Niwe mkweli  Yanga hawajatulipa pesa yetu ndio maana nikamwambia Kindagule aendelee kutuvumilia tulipipwa na Yanga na sisi tutawalipa pesa yao”alisema Kiongozi huyo.

 

  Alipoulizwa tena kwa nini wamekubali kumtoa Kipa wao Muhimu bila kulipwa pesa ili hali wakijua mchezaji huyo sio mali yao peke yao kuna taasisi iliyoibua na kukuza kipaji chak.?

 

 Kiongozi huyo hakujibu swali hilo na badala yake alikata simu.

 

 

Siku za nyuma sakata hilo liliibuka kweny vyombo vya habari ambapo Uongozi wa yanga urikaririwa ukidai kwamba umesharipa malipo ya Kipa huyo na hawadai chochote.

 

Baadhi ya wachezaji wa Moro Kids waliotimkia timu mbali mbali zikiwemo Simba na Yanga waliouzwa na Mtibwa Sugar ni Pamoja na Shomari Kapombe, na Mzamiru Yasini Simba.

 

 Dickson Job, Shomari Kibwana na Kipa Abuutwarib msheri[Yanga] Shiza Kichuya, [Namungo].Hassan Kessy[KMC] Juma Abdul Singida Big Stars na Hamad Waziri’Kuku [Mbeya City]

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...