Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Monday, May 9, 2022

ABOOD ACHANGIA UJENZI WA JENGO LA WANAHABARI MORO.

Mgeni rasm Mh Azizi Aboodkati[ akiwa na wenyeji wake Mwenyekiti wa chama cha Waandishi wa habari Mkoa wa Morogoro Nickson Mkilanya[kulia]na Katibu Mkuu wa chama hicho Lilian Lucus Kasenene
Baadhi ya Wanandishi wa habari pamoja na Wanafunzi wa Vyuo vya uwandishi wa habari wakimsikiliza mgeni rasm
.....Mh Abood aakitoka ukumbini huku akisindikizwa na Mwenyeji wake Mkilanya


Mh nAbood akipiga Picha na Waandishi wakongwe wa Mkoa wa Morogoro
Mwenyekiti wa Cha =ma Cha Waandishi wa habari Mkoa wa Morogoro Nickson Mkilanya kushoto. akizungumza na Mh Abood mara baada ya haffa hiyo kutamatika ukumbi wa Savoy
Katibu Mkuu wa Cha cha Waandishi wa habari Mkao wa Morogoro Lilian Lucus Kasenene Kulia akizungumza na Mh Abood

Mwanfishi Mwandamizi wa Magazeti ya Mwananchi Mkoa wa Morogoro Madam Hamida Shariff akitoa maelekezokwa muhudumu wa chakula



 Mtangazaji Mkongwe nchini Bujaga lzengo Kadako'Baba Askofu' akichukua Menyu kwenye hafra hiyo. lfahamike Mzee Kadako aliwahi kutanagza Redio Tanzania kwa sasa TBC LTV na badaye akaja Moro kujiunga na Abood Media kabla ya kutimkia SUA Media pia ya Morogoro ambapo aliduku huko mpaka alipostaafua hivi karibuni


                       Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

 MBUNGE wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh Aziz Abood ameahadi kuchangia Ujenzi wa Jengo la kisasa la Chama Cha Waandishi wa habari Mkoa wa Morogoro’MOROPC’ linalojengwa eneo la Kimbwe Juu ya Milima ya Uluguru Jirani na Ofisi ya Wamo Mkoa wa Morogoro.

 

Mh Abood ambaye pia ni Mfanyabiashara Maarufu nchini Tanzania akimiliki Viwanda, Mabasi, Malori na Vyombo vya habari alitoa ahadi hiyo jana kwenye Maadhimisho ya Vyombo vya habari duniani yanayofanyika kila mwaka Mei 3.

 

 Waandishi wa Morogoro waliradhimika kufanya maadhimisho hayo jana Mei 9 kwenye Ukumbi wa Savoy kufuatia Viongzoi wao wa ngazi za juu kushiriki kwenye madhimisho hayo yaliofanyika Kitaifa Jijini Arusha yalihudhuriwa na Vyama vya waandishi wa habari kutoka nchini zote 54 za Afrika na mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo yaliyofanyika Mei 3 alikuwa Rais Samia Suluhu Hassan’Maarufu Mama Samia.’

 

 Waandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali vya habari Mkoa wa Morogoro walishiriki kwenye maadhimisho hayo yaliyohudhuriiwa pia na wanafunzi wa vyuo mbali mbali vya Uandishi wa habari  Mkoa wa Morogoro kikiwemo Chuo Pendwa cha Morogoro School Of Journalisim’M.S.J’ Chuo ambacho kimetoa Waandishi wengi wa habari maarufu nchini akiwemo Mwandishi wa wa habari hizi.

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...