Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Friday, November 12, 2021

KUFUATIA UKAME MTO MOROGORO WANYAUKA MORUWASA WATO NENO KWA WATEJA WAO.


Watu wametumia fursa hiyo kuchimba mchanga mtoni jambo ambalo ni uhalibifu wa mazingira


                    Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

WAKATI Wakuu wa nchini mbali mbali duniani ikiwemo Tanzania wakishiriki Mkutano wa Majadiliano ya  Mabadiliko ya Tabia Nchini uliofanyika Nchini Poland, habari ikufikie kwamba baada ya kupita miaka Mingi Mto Mkuu wa Morogoro umenyauka kwa Ukame.

 

Jana Mwandishi wa Mtandao huu aliyekua akiangalia gemu kati ya timu ya  Tanzania’Taifa Star’ dhidi ya Congo DR. kwenye Baa ya Top Ten iliyopo Mtaa wa River Side Kata ya Mwembesongo  Mkoani hapa.

 

Wakati wa Mapunziko Mwandishi huyo aliamua kuzunguka nyuma ya baa hiyo kupunga Upepo kando kando ya Mto huo na kushuhudia Mto huo umenyauka kwa kiasi kikubwa hali iliyopelekea baadhi ya wanchi kuvamia na kuchimba Mchanga kwa lengo la kwenda kufanya shughuli za Ujenzi kama inavyoonekana kwenye moja ya Picha.

 

Kwa sasa Maeneo Mengi nchini ikiwemo  Morogoro Jua ni kali Mno Sambamba na Joto kali nyakati zote asubuhi, Mchana na Usiku.

 

Kufuatia hali hiyo  Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Jiji la Dar’DAWASCO’ hivi karibuni walitangaza Mgao wa Maji kwenye jiji hilo la Maraha ambalo baadhi ya vyanzo vyake vya Maji vinatoka Mkoa wa Morogoro.

 

Leo  Muda huu Mwandishi wa habari hizi ambaye ni mteja wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Mkoa wa Morogoro’MORUWASA’amepokea Ujumbe kwenye simu yake kutoka MORUWASA unaosema.

 

”MORUWASA Inapenda kuwataarifu kutokana na hali ya Ukame kumekuwa na Changamoto za Uzalishaji  kwenye Vyanzo vyake vya Maji na hivyo kuathri upatikanaji wa Maji eneo kubwa linalohudumiwa.

 

MORUWASA inawashauri wateja wake kutumia kwa uangalifu kiasi cha Maji kinachowafikia -tushirikiane kulinda vyanzo vya Maji kwa huduma endelevu”Mwisho wa Kunukuu Ujumbe huo  hadi muda huu bado upo kwenye simu yangu.

Kwenye hili hakuna Mwananchi yoyoye atakayekuwa na Malalamiko kwa Mamlaka hizo za Maji nchini kwani kila mtu anaona hali hali ya Ukame kwa vile si watu wote ni wateja wa MORUWASA  Mtandao huu umeamua kuweka ujumbe huo wa MORUWASA kwa lengo la kuwasilisha kwa wadau wa Matndao huu ambao sio wateja wa MORUWASA ingawa wanatumia Maji ya Mamlaka hiyo.


 

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...