Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Sunday, October 24, 2021

WAKALI WA NYIMBO ZA INJIRI NCHINI WENGI WAO WANATOKEA MKOA WA MBEYA

 Bahati Bukuku akimkabidhi Kipaza sauti’Mic’ Mchungaji Emmanuel Mgaya Maarufu Masanja  Mkandamizaji’ ambaye pia ni Msanii Maarufu wa vichekesho chini akipiga kazi kundi la Original Commedy. 



Na Dunstan Shekidele,Morogoro.  

Kila Mkoa hapa nchini unasifa zake za kutoa wasanii wengi wa fani mbali mbali kama vile Soka, Riadha Muziki wa bongofleva Nyimbo za lnjiri na Uigizaji.

 

Mkoa wa Morogoro unaongoza nchini kwa kuzalisha wachezanyo wengi wa Mpira wa Minguu nchini wanaotamba timu mbali mbali zikiwemo Simba, Yanga na Azam.

 

Mkoa wa Arusha unaongoza kwa kuzalisha wachezaji wengi wa Riadha Wazee wa Kukimbiza Upepo’ Mkoa wa Kigoma unaongoza kwa kusambaza wanamuziki nyota wa Bongofleva kama vile Nassib Abdul'Diamond Platnums’ Ally Kiba, Ommy Dimpoz na Mikoa ya Dar es salaam na Pwan yenyewe inaongoza kuzalisha Waingizaji wa Filam na Vichekezo.

 

Hii na Chomekea Mkoa wa Mara wenyewe unaongoza kutoa wapiganaje’Wanajeshi’ wengi kwenye kambi nyingi za Jeshi nchini.

 

 

Wadau mtandao huu mtakubaliana nami  kwamba kwa sasa hapa nchini Mkoa wa Mbeya ndio unaongoza kwa kutoa waimbaji wengi nyota wa nyimbo za lnjiri.

 

Miongoni mwa waimbaji hao ni pamoja na Bahati, Bukuku[kulia]Matha Mwaipaja]Kati] na Stara Thomas, kwa pamoja Mastaa hao wakipozi mbele ya Kamera za Mtandao huu kwenye moja ya Tamasha la lnjiri lililofanyika Uwanja wa Jamhuri Morogoro.

 

Kwa stara Thomas sijang’amua Mara Moja mkoa anaotoka.

                                 CAPTION

 

 PICHA YA KATI JUU

Mwandishi wa Mtandao huu kulia akimuweka Mtu kati Msanii nyota wa lnjiri[Muziki wa kumtukuza Mungu’ na Muziki wa kizazi Kipya’Bongofleva’ Stara Thomas.

Kwenye mahojiano hayo aliulizwa swali, kwa nini anakuwa vuguvugu Moto si Moto baridi si baridi kwa maana  mchana anaimba nyimbo za kumtukuza Mungu nyimbo za lnjiri na Usiku anaimba nyimbo za Bongofleva nyimbo za kidunia,kwamba  kiimani jambo hilo limekaa kaaje?

 

Swali hilo lilionekana kumzidi kimo Msanii huyo ambapo  alipotakiwia  kujibu muda mwingi aliutumia kuchezea macho yake na mwisho akajibu kwa kifupi akisema.

 

” Swala hilo limekaa vibaya so muda wowote kuanzia sasa nitaachana na muziki wa kidunia na kubaki kwenye kazi Moja ya kumtumikia Mungu wangu ambaye ni Mwaminifu kwangu”

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...