Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Monday, July 26, 2021

GEMU YA SIMBA -YANGA, MASHABIKI SIMBA WAVAMIA TAWI LA YANGA.

Wanachama na Mashabiki wa Simba wakifuatilia kwenye Luninga gemu ya Simba na Yanga jana
Mwenyekiti wa Tawi kuu la Yanga Mkoa Morogoro lssa Chabala akiwatumia maneno ya Shombo Mashabiki wa Simba waliovamia tawi hilo mara laa ya timu yao kuinyuka Yanga bao 1-0
Baada ya kutoka tawi la Yanga Mashabiki hao walitinga Mitaa ya Mwembesongo wakiwa na khanga iliyoandikwa Simba Bingwa
Shabiki kindaki ndani wa timu ya Simba ambaye ni Mwanachama wa tawi la Shujaa Morogoro Maarufu Haji Manara ya Morogoro, aliongoza Maandamano hayo akiwa na duraha kama yote ya kumfunga Mtani wao, Shabiki huyo akipozi mbele za Kamera ya Mtandao huu maeneo ya shule ya Msingi Mwembesongo

 


Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

BAADA ya timu yao kulipa kisasi Mashabiki wa Simba wamevamia tawi kuu la Yanga la Mkoani Morogoro, huku wakiimba nyimbo  zinazotaja jina la Mzee Mpili.

 

Kundi hilo la Mashabiki wa Simba wake kwa waume Vijana kwa Wazee, Mara baada ya Simba kukata ‘ngebe’ za Mzee Mpili kwenye mchezo wa fainali ya Michuano ya Azam Federation Cup uliopigwa jana Uwanja wa Lake Tanganyika Mkoni Kigoma.

 

 Kukamilika kwa Mnyama Simba kuitandika Yanga bao 1-0,kundi hilo la Mashabiki wa Simba walianza Maandamano yao yasio na kibali cha Polisi  kuanza kwenye tawi kuu la timu hiyo lililopo Mji Mpya jirani na Soko na kuendelea kwenye tawi kuu la watani zao Yanga lililopo pia Mji Mpya jirani na Stend ya Daladala wakisema nyinyi mmetupiga ngumi ya mgongoni ambayo haina Point sisi leo tumewatandika ngumi ya Kichwani ambayo imetupatia kombe na Pesa.

 

Licha ya maneno hayo ya ‘Shombo’ waliokwenda Sambamba na Machungu ya Kufungwa lakini Mashabiki hao wa timu ya Wananchi’Yanga’ walikuwa kimwa wakinywa Tangawizi, kahawa na Kashata.

 

Huku Mwenyekiti wa Tawi hilo lssa Kitukwa’Maarufu lssa Chabala’akijibu Mapigo naye akiwakera Mashabiki hao wa Simba akisema “Mwaka huu tumewapiga Mara mbili Kule Zanzibar na juzi tarehe 3 pake kwa Mkapa, leo tumewachia ili amani irejea kwenye timu yenu kama tungewafunga Mngemfukuza Haji Manara mkimshutumu kwamba ana urafiki na bosi wetu GSM tukutane kwenye Ngao ya hisani mwezi ujao”alisema Mwenyekiti huyo wa tawi kuu la Yanga Mkoani Morogoro.

 

Baada ya maneno hayo Kundi hilo la Mashabiki wa Simba liliondoka kwenye tawi hilo Mwandishi wa Mtandao huu aliyeweka kambi kwenye matawi hao ya Simba na Yanga ambayo yako jirani jirani yakitenganishwa na mitaa miwili peke wake aliweka Kambi kwenye Matawi hayo akisaka stori za Chini ya Kapeti.

 

Baada ya nusu saa ndoka kundi hilo la Simba kuondoka kwenye tawi hilo la Yanga,  ghafla Mwenyekiti wa Tawi kuu la Simba Mkoani Morogoro ‘Maarufu tawi la Shujaa’ Bw Saidi Mkwinda alitinga kwenye tawi la Yanga na kumvamia Mwenyekiti wa tawi hiyo lssa Chabala nini kilitoea endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote.

                            

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...