Sanamu lenye mfano wa Sadio Mane limejengwa nchini kwao Senegal......Mane akipongezwa na wenzake huku wakimtwisha kombe kichwani Mane akiwa na familia yake
Na Dunstan
Shekidele.Morogoro.
FAINALI za
Mataifa ya Afrika'AFCON' zilizoanza kutimua vumbi nchini Morocco Disemba 21 na kutamatika January 18 kwa Senegal
kutwaa ubingwa akiwanyuka wenyeji
Morocco kwa bao 1-0.
Morocco walijikuta wakitoka uwanjani vichwa
chini huku wengine wakimwaga machozi kwa uchungu wa kulikosa kombe ndani ya
ardh yao ya nyumbani.
Wachezaji
wengi wa Morocco walitinga uwanjani na familia zao kwa lengo la
kupiga picha nazo wakiwa na kombe hilo.
Hali
ilibadilika walijikuta wakiwa shuhudia wachezaji wa Senegal wakinyakua mwali
huyo na kupiga naye picha na familia zao huku wachezaji wa Morocco wakienda
nunia kwao baada ya kuwanyiwa ubaya na ubwela na Senegal ya Sadio ‘Pesa’ Mane
Mara baada
sherehe hizo kutamatiza Nahodha wa Senegal Mstaarabu Sadio Mane alizungumza na
waandishi wa habari.
Kwenye
mazungumzo hayo Mane. Pichani na familia yake alisema maneno yaliyojaa hekima,Utu
na busara.
"Huu
ushindi ni wa Waafrika wote waliokuwa wakituunga mkono"
Mwafrika
kutoka Afrika Mashariki na Kati nchi Pendwa ya Tanzania Dustan Shekidele
alikuwa mmoja wapo aliyeiunga mkono Senegal kwenye Fainali hiyo uku akiiombea mabaya
Morocco wafungwe.
Kama lpo lpo
na riziki ya mtu haizuiwa bali inacheleweshwa tu, licha ya refa Mkongo Man
kuonyesha dhairi kuibeba Morocco kiasi cha Kocha wa Senegal kuamua kususia
mchezo huo baada ya refa huyo kuipa Pelnaty Morocco dakiza za mwisho mwisho za
mchezo huo.
Hata hivyo
Sadio Mane aliyebaki peke yake uwanja baada ya wenzake 10 kususi mchezo huo na
kutoka uwanjani wakikimbilia vumbani.
Mane
aliwafuata wenzake na kuwasihi warejee uwanjani.wachezaji hao walimtii Nahodha
wao huyo na kurejea uwanjani baada ya gemu hiyo kusimama kwa takribani dakika
10.
Waliporejeja
zikiwa zimesalia takribani dakika 7 mchezo huo kutamatika Morocco walipiga
ichani hiyo ambapo kw amshanga wawengi mchezo wa Morocco alipiga kishuti ‘Mtoto’
kilichodakwa na kipa wa Senegal Mendy.
Dakiza za
magharibi ya roho zakika za mwisho Mwamba Sadio Mane alifunga bao lililodumu
hadi mwisho wa mchezo.
Ikumbukwe fainali za kombe la Dunia zilizofanyika
nchini Qatar mwaka 2022 na wawakishiri wa bara la Afrika Morocco kuweka rekodi
ya kutinga Nusu fainali ya michuano hiyo.
Kocha mkuu
ww Morocco akizungumza.na waandishi wa habari alisema.
Mafanikio
hayo waliyotapata ni kwa wananchi wa Morocco na sio kwa wafrika.
Kauli hiyo
ilizua mjadala mzito barani Afrika.kufuatia hali hiyo uongozi wa juu wa Morocco
ulijitokeza hadharani na kupinga kauli hiyo.
Ukikanusha
maneno hayo ya kocha wao uongozi huo ulisema kauli hiyo si ya wana Morocco bali
ni kauri binafsi ya kocha.
Maneno hayo
yalipunguza machungu ya waafrika wengi waliokuwa
wakiisapoti timu hiyo kwenye michuano hiyo mikubwa duniani.