Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Friday, May 27, 2022

KUMBUKIZI YA MIAKA 8 YA MSANII ALBERT MANGWEHA.


 


 

Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

 

 Mei 28 -2013 Mkali wa Muziki wa Hip Hop nchini Albert Keneth Mangweha’Ngwea’ alifariki dunia  nchini Afrika Kusini na kuzikwa wiki iliyofuata Mkoani hapa, hivyo  leo mei 28-2022 Msanii huyo ametimiza miaka 9 toka alivyoiaga dunia.

 

Famila ya Hayati Mangweha inayoishi Kihonda Mtaa wa Mazimbu Road Morogoro anafanya lbada ya kumuombea mpendwa sambamba na kudhuru kwenye kaburi la Msanii huyo lililopo nje ya kanisa Katolini Jimbo la Morogoro Parokia ya Mt Monica Kihonda.

 

  Mtandao huu leo unakamirisha matukio ya Kifo cha Msanii huyo Kipenzi cha wengi kwa tukio la Msanii mwenzake Kala Jeremiah kudhuru kwenye kaburi la Ngwea kisha kutinga nyumba na kumkabidhi Mama Tuzo Mama Mangweha.

 

 Mara baada ya  kutwaa tuzo 3 kwa mpigo  za Kili Music Award 2013 Msanii wa Miondoko ya Hip Hop nchini,Kala Jeremiah baada ya kukabidhiwa Tuzo hizo Msaani huyo alifunga safari kitoka Dar Mpaka Moro  na kudhuru kaburi la Ngwea akiwa na Tuzo hizo 3.

 

 

 

Baada ya kutoka makaburini akiwa na Mwandishi wa habari hizi alitinga nyumbani kwa Mama Mzazi wa  ‘Ngwea’ Bi Denisia Mangweha na kumkabidhi tuzo moja kama ishara ya  kutambua mchanga wa Msanii mwenzake huyo aliyetangulia mbele za haki.

 

 

Kwa uchungu Bi Mkubwa huyo mara baada ya kupokea Tuzo hizo aliangua kilio akimkumbuka Mpendwa Mtoto wake Mara baada ya kukamilika kwa zoezi hilo lililofanyika nyumba kwa Mama huyo Mtaa wa Mazimbu Road, Mwandishi wa habari hizi alipata wasaha wa kuzungumza na Msanii huyo ambaye kwa sasa yuko kimya sana kimuziki.

 

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...