Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Friday, February 27, 2026

HABARI KALI YA KIJAMII WIKI HII NI HAKI MTOTO MCHANGA KUNYWA DAWA HUKU ANA NYONYA MAZIWA YA MAMA?


                    Dr Sadick akizungumza na Mtandao huu


                 Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

IMEZOELEKA kitabibu Mtu anapougua na kupewa dozi ya dawa, hushauri na daktari asinywe maziwa mpaka atakapomalizi dozi.

 

Hali hii imeonekana kuwa tofauti kwa kundi la watoto wachanga ambapo utafiti wa awari uliofanywa na Mwandishi wa habari hizi umebaini watoto wengi wachanga ambao chakula cha kikuu ni Maziwa ya Mama wanapougua hupewa dozi za dawa huku wakiendelea kunyonya maziwa ya mama zao.

 

Wiki iliyopita Mwandishi wa habari hizi akiwa kwenye kikao cha kikundi mfla cha ‘kikobe’alimshuhudia Mwanamke mmoja mwanakikundi akimpa dawa Mtoto wake mchanga.

 

Baada ya kumnywesha dawa hiyo Mtoto huyo alianza kuangua kilio kwa uchungu wa dawa, hivyo Mama huyo aliamua kumnyamazisha  kwa kumnyonyesha.

 

Kufuatia hali hiyo Mtandao huu alimuliza Mama huyo iweje amempa dawa mtoto na Muda huo huo ana mpa maziwa?

 

Mama huyo alijibu.”Watoto wachanga mara nyingi wanaugua mara kwa mara na chakula chao kikuu ni haya maziwa yetu binafsi Clinc sijashauriwa kuacha kumnyonyesha mtoto pale ninapompa dawa” alisema Mama huyo ambaye jina lake linahifadhiwa kwa sababu maalumu.

 

Kufuatia majibu hayo Mwandishi wa habari hizi jana aliamua kumtafuta Daktari kwa lengo la kutapa majawabu ya jambo hili huyo hapa Daktari Sadick Juma.

“ Swali zuri sana iko hivi kwa ukuu wa Mungu Maziwa ya Mama nitofauti na Maziwa mengine Maziwa ya binadamu yana Virutubisho na Kinga hivyo Maziwa hayo hayauwi nguvu ya dawa ili kuthibitisha hilo ndio maana mama anapokuwa na maradhi ya kuambukizi huwa tunamshauri asimnyonyeshe mtoto”alisema Dr Sadick  na kuongeza.

 

Kweli huwa tunashauri kwa mtu mzima au mtoto wa umri wowote anapomeza aina ya daiwa asitumie maziwa ya wanyama kwa sababu dawa nyingi zina Hasid hivyo maziwa hayo huuwa nguvu ya dawa.

 

Katika kuongezea hilo sumu nyingi zina Hasid tumeshuhudia mara  kadhaa mtu akinywa Sumu akiwahiswa kupewa Maziwa anapo hii ni kwa sababu Sumu nyingi zina Hasid hivyo zikikutana na Maziwa zina zina kosa nguvu.

 

Ila kuna dawa nyingine hazina Hasid kama vile Mseto unaweza kumeza huku unakunywa maziwa haina shida yoyote”alisema Daktari huyo kutoka hospital ya Wahindi ya Ahhamadiya iliyopo katikati ya Mji wa Morogoro.  

                  


 

 

Monday, February 23, 2026

WATU MASHUHURI WALIOSHIRIKI MAZISHI YA BABA MZAZI WA BEKI WA SIMBA.

 

Beki wa Simba Abdulrazack Spear Hamza mwenye Flana nyeusi [kulia] akizungumza na ndugu na jamaa waliomkimbilia kwenye msiba huo mzito wa Mpendwa baba yake hayati Spear Mohamed Hamza.

Mansoor Chamchua ‘Mzee wa Bums’ambaye ni Swahiba Mkubwa wa Rais wa shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania’TFF’ Wales Karia, akisalimiana na Faudhi Al-Saed ‘Maarufu Micho’ambaye baba yake mzazi ndiye Mmiliki wa mabasi ya Kampuni ya Al-Saed.

Faudhi Micho akimtania Mpiga picha wa Mtandao baada ya kumshuhudia akiwaphotoa picha hizi.

Shehe Omar Ally ambaye ni Mhadhini Mkuu wa Msikiti Mkuu wa Morogoro ambaye pia ni Mshauri wa Mufti, ndiye aliyetoa mawaidha kwenye msiba huo.

Geofrey Job Maarufu Jofu Job[kulia] mwenye kofia] ambaye ni baba mdogo wa beki kisiki wa Yanga Dickson Nickson Job akibadilishana mawazo na Mhe diwani wa Kata ya Saba saba Mohamed Lukwele[kati] ambaye baraza la madiwani lililopita alikuwa Naibu Meya, kushoto anayezungumza ni Mlapakolo.

Shehe Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Shehe Jafar Sineli

 Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Morogoro Nickson Mkilanya[kulia] akiwa msibani hapo na Diwani wa Kata ya Kihonda Maghorofani Mhandisi  Hamis Ndwata ambaye pia ni mmoja wa Madiwani waliogombea kiti cha Umeya wa Halmashauri ya Mji wa Morogoro laki kura hazikutoka na nafasi hiyo kunyakuliwa na Khalid Matengo diwani wa kata ya Mji Mkuu.

Shabiki Maarufu wa Simba Mkoa wa Morogoro Hussen Kilimo anayefanya shughuri za kusafisha viatu jirani na mzunguko wa barabara uliopo katikati ya Mji wa Morogoro jirani na stend ya zamani ya daladala ambayo kwa sasa imegeuzwa kuwa maegesho ya magari naye alikuwepomsibani hapo.


 

Gari lililobeba mwili wa hayari Spear likikatiza katikati ya uwanja kuelekea makaburi ya Magadu nje kidogo ya Mji wa Morogoro.

Abdulrazack alianza kuibua kipaji chake cha soka kwenye uwanja huu, kauli hii aliitoa hayati Spear alipohojiwa na Mtandao huu enzi za uhai wake.

MAJAJI 2 WAHUDHURIA IBADA YA KUMUOMBEA KIGOGO WA SUA MAREHEMU DKT MBILU.

         Mchungaji Dkt Rhoda Chamshama akiongoza ibada hiyo Katibu Mkuu wa  KKKT Usharika wa Mji Mpya Mshana akimuaga Mzee wake wa kanisa S...