Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Thursday, January 29, 2026

KIJIWE NONGWA. UKIONA KAFUTA BANGO UJUMBE UMEFIKA


Na Mpekunyuzi wa Mitandaoni Dunstan Shekidele.

Kama kawaida mtumishi wako, kila wiki naweka Bando linalonitembeza kwenye Mitandao ya Kijamii kukusanya jumbe mbali mbali.

Miongoni mwa jumbe hizo ni za Kuelimisha, Kukosoa na Maneno ya hekima yanayotukumbusha kutenda mambo  mema.

Kwa jumbe nyingine mbali mbali tukutane wiki ijayo panapo majaliwa ya Mwenyezi Mungu















 

Tuesday, January 27, 2026

WANANCHI MORO WAFUNGUKA ,MAZITO KWENYE JUMBE WALIZOANDIKA KWENYE VYOMBO VYAO VYA USAFIRI.

                        Boda boda Mstaarabu Lamia Abdallah
                            Mjasiliamali Mdogo Stetephen  Philipo

 

    Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

WANANCHI Wawili mkoani Morogoro,Stephen Philipo na Lamia Abdallah wameamua kutema nyongo kwenye Jumbe walizoweka kwenye vyombo vyao vya usafiri.

 

Mtandao huu ukiwa kwenye pilika pilika zake za kusaka matukio mitaani ulimshuhudia Limia Abdallah ambaye ni dereva wa boda boda anaye ‘Pack’ boda boda yake Soko la Chief Kingalu akiandika ujumbe unaosomeka hivi ‘Janja la Kutafuta Jinga la Kuhonga’.

 

Mara baada ya kumpiga picha Mtandao huu ulizungumza naye na mahojiano hayo yalikuwa hivi.

Mwandishi. Habari yako Afisa usafirishaji.

Lamia. Hoo safi Shekidele Mwandishi bora Morogoro nambie.

 

Mwandishi.Poa, kwa nini umeandika ujumbe huu umemfumbia mtu au una kuhusu wewe mwenye?

 

Lamia. Unanihusu mimi mwenyewe, ni kweli nambambani sana kutafuta pesa lakini mwisho wa siku matumizi ya hizo pesa ni kuhonga.

 

Mwandishi. Una mke?

Lamia. Ndio.

Mwandishi.Kwa nini sasa unakuwa Jinga la kuhonga ili hali una mke?

 

Lamia. Haa Shekidele hizo pesa za matumizi ninazo mpa mke wangu sindio na honga,maana ya ujumbe huu ni kwamba napambana kutafuta pesa kwa lengo kuu la kutunza familia yangu na si vinginevyo.

 

Mwandishi. Kutunza familia sio kuhonga nio kuhudumia kuhonga mara nyingi imezoeleka kumpa pesa hawara a.k.a mchepuko.

 

Lamia. shekidele kumpa pesa Mwanake yoyote awe mke wako au sio mke wako ni kuhonga tu hujaona mtu anamuhudumia mkewe wake mwisho wa siku huyo mwanamke anamkimbia sasa anakwenda kwa mwanaume mwingine ,kuhudumia ni kwa mzazi wako ambaye hawezi kukukimbia hata kama ukifirisika.

 

Mwandishi, Du haya bhna ila binafsi sikubaliani na hoja zako hizo.

 

Lamia. Sawa Shekidele unauhuru wa kukubari au kutokubali lakini yangu ndio hayo.

 

Siku iliyofuata Mtandao huu ulikutana na

Steven Philipo Soko la Mji Mpya ambaye mbele ya baiskeli yake aliweka bango lenye ujumbe unaosomeka hivi ‘Shida ingekuwa Sumu tungekufa wengi’ nikamuliza kwa nini umeandika hivyo majibu yake haya hapa.

 

“ Namshangaa sana Mungu yaani Broo mimi ninashida nyingi sana lakini nashangaa sifi, kama shida zinaua basi tungekufa wengi”alisema Philipo na kuongeza.

 

“Kwa ukumbwa na jambo hilo licha ya shida zangu niliamua kwenda Stationary nikatoa buku langu kuandika ujumbe huu kueleza ulimwengu”alimalizia kusema jamaa huyo ambaye anafanya biashara ya kuua Matango na Mihogo ya kutafuna.


 

Sunday, January 25, 2026

FAINALI ZA AFCON 2025.KAULI YA SADIO MANE NI YA KIUNGWANA.

Sanamu lenye mfano wa Sadio Mane limejengwa nchini kwao Senegal
......Mane akipongezwa na wenzake huku wakimtwisha kombe kichwani
                               Mane akiwa na familia yake


Na Dunstan Shekidele.Morogoro.

FAINALI za Mataifa ya Afrika'AFCON' zilizoanza kutimua vumbi nchini Morocco  Disemba 21 na kutamatika January 18 kwa Senegal kutwaa ubingwa akiwanyuka  wenyeji Morocco kwa bao 1-0.

 Morocco walijikuta wakitoka uwanjani vichwa chini huku wengine wakimwaga machozi kwa uchungu wa kulikosa kombe ndani ya ardh yao ya nyumbani.

Wachezaji wengi wa Morocco walitinga uwanjani na familia zao  kwa lengo la  kupiga picha nazo wakiwa na kombe hilo.

Hali ilibadilika walijikuta wakiwa shuhudia wachezaji wa Senegal wakinyakua mwali huyo na kupiga naye picha na familia zao huku wachezaji wa Morocco wakienda nunia kwao baada ya kuwanyiwa ubaya na ubwela na Senegal ya Sadio  ‘Pesa’ Mane

Mara baada sherehe hizo kutamatiza Nahodha wa Senegal Mstaarabu Sadio Mane alizungumza na waandishi wa habari.

Kwenye mazungumzo hayo Mane. Pichani na familia yake alisema maneno yaliyojaa hekima,Utu na busara.

"Huu ushindi ni wa Waafrika wote waliokuwa wakituunga mkono"

Mwafrika kutoka Afrika Mashariki na Kati nchi Pendwa ya Tanzania Dustan Shekidele alikuwa mmoja wapo aliyeiunga mkono Senegal kwenye Fainali hiyo uku akiiombea mabaya Morocco wafungwe.

Kama lpo lpo na riziki ya mtu haizuiwa bali inacheleweshwa tu, licha ya refa Mkongo Man kuonyesha dhairi kuibeba Morocco kiasi cha Kocha wa Senegal kuamua kususia mchezo huo baada ya refa huyo kuipa Pelnaty Morocco dakiza za mwisho mwisho za mchezo huo.

Hata hivyo Sadio Mane aliyebaki peke yake uwanja baada ya wenzake 10 kususi mchezo huo na kutoka uwanjani wakikimbilia vumbani.

Mane aliwafuata wenzake na kuwasihi warejee uwanjani.wachezaji hao walimtii Nahodha wao huyo na kurejea uwanjani baada ya gemu hiyo kusimama kwa takribani dakika 10.

Waliporejeja zikiwa zimesalia takribani dakika 7 mchezo huo kutamatika Morocco walipiga ichani hiyo ambapo kw amshanga wawengi mchezo wa Morocco alipiga kishuti ‘Mtoto’ kilichodakwa na kipa wa Senegal Mendy.

Dakiza za magharibi ya roho zakika za mwisho Mwamba Sadio Mane alifunga bao lililodumu hadi mwisho wa mchezo.

 

Ikumbukwe  fainali za kombe la Dunia zilizofanyika nchini Qatar mwaka 2022 na wawakishiri wa bara la Afrika Morocco kuweka rekodi ya kutinga Nusu fainali ya michuano hiyo.

Kocha mkuu ww Morocco akizungumza.na waandishi wa habari alisema.

Mafanikio hayo waliyotapata ni kwa wananchi wa Morocco na sio kwa wafrika.

Kauli hiyo ilizua mjadala mzito barani Afrika.kufuatia hali hiyo uongozi wa juu wa Morocco ulijitokeza hadharani na kupinga kauli hiyo.

Ukikanusha maneno hayo ya kocha wao uongozi huo ulisema kauli hiyo si ya wana Morocco bali ni kauri binafsi ya kocha.

Maneno hayo yalipunguza   machungu ya waafrika wengi waliokuwa wakiisapoti timu hiyo kwenye michuano hiyo mikubwa duniani.


 

Wednesday, January 21, 2026

LOVE IS A POLSON.[KUPENDA NI SUMU]










 

   

HUENDA kuna ukweli kwamba kupenda kitu au Mtu ni kama sumu,

 

Ligi ya Mabingwa barani Ulaya imeendelea jana usiku huku mashabiki wengi duniani wakitupia jicho gemu kubwa ya Inter Milano ya Italia na Arsenal ya England.

 

Kwa saa za Tanzania gemu hiyo ilianza majira ya saa 5 usiku na kutamatika saa 7, kwa mapenzi ya mchezo wa Soka mashabiki wengi waliamua kukesha kuangalia gemu hiyo iliyotamatika kwa chama bora duniani kwa sasa Arsenal washika bunduki wa jiji la Maraha la London kuwanyuka wenyeji wao kwa chuma 3-1.

 

Miongoni mwa mashabiki hao ni shabiki ‘lia lia’ wa Arsenal  Dunstan Shekidele’Ez Come Ez Go’ alikesha na kikombe cha kahawa akicheki gemu hiyo kwenye Hotel ya Glonency iliyopo Nane Nane Kando kando ya barabara kuu ya Morogoro-Dar –es-salaam jirani kabisa na uwanja wa maonyesho ya wakulima Nane nane Kanda ya Mashariki.

 

pIchani Shekidele aliyetinga jezi Mpya ya Arsenal akimshuhudia mshambuliaji wa Arsenal Gabril Jesus akipachika mabao 2 kwenye ushindi huo wa bao 3,

 

lfahamike Jesus ambaye ni Raia wa Brazil kwa kipindi kirefu alikuwa nje ya uwanjani akiuguza majeraja kwa sasa amerejea na Moto wake ule ule.

 

Mpiga picha wa Mtandao huu akitumia kamera ya kisasa alifanikiwa kunasa magori hayo 2 kwenye Luninga kubwa ya hotel hiyo kama anavyoonekana pichani Jesus jezi namba 9 akimtungua mara 2 kipa wa lnter Milano.

 

MAJAJI 2 WAHUDHURIA IBADA YA KUMUOMBEA KIGOGO WA SUA MAREHEMU DKT MBILU.

         Mchungaji Dkt Rhoda Chamshama akiongoza ibada hiyo Katibu Mkuu wa  KKKT Usharika wa Mji Mpya Mshana akimuaga Mzee wake wa kanisa S...